Monday, May 8, 2017

SIMULIZI, NILIKIONA CHA MOTO URITHI WA BABU SEHEMU YA 23

ZULIA LA FAKI
 
NILIKIONA CHA MOTO URITHI WA  BABU 23
 
ILIPOISHIA
 
Kitu ambacho kilitushangaza zaidi mimi na Inpekta Amour ni kuwa tarehe ile ile ya usajili wa mara ya pili ndiyo tarehe hiyo hiyo ambayo Ummy alianza kunipigia simu. Kumbukumbu za tarehe  zilikuwa bado zipo kwenye simu yangu.
 
“Sasa tunaomba utupatie namba nyingine ambazo zilimekuwa zikiwasiliana na namba hii” Inspekata Amour akatoa ombi jingine.
 
Msichana baada ya kuangalia kwa makini alisema.
 
“Hii namba tangu iliposajiliwa kwa mara ya pili rekodi yake inaonesha kuwa iliwasiliana  na namba moja tu”
 
Alipoitaja namba hiyo ilikuwa ni namba yangu mimi.
 
Amour akanitazama kwa mshangao kabla ya kuuliza swali jingiine.
 
“Ilifanya mawasiliano mara ngapi?”
 
“Mara tano”
 
SASA ENDELEA
 
Inspekta Amour akanigeukia mimi.
 
“Mlifanya mawasiliano mara tano?” akaniuliza.
 
“Nafikiri inaweza kufika mara tano”
 
“Inaonekana kama aliifufua namba yake ili kukupigia wewe tu”
 
“Sasa swali, katika kipindi chote cha miaka mitano alichoacha kutumia hii namba alikuwa wapi?”
 
“Ndicho hicho kipindi anachodaiwa kuwa alikufa lakini usajili wake unaonesha kuwa hakuwa amekufa miaka mitano iliyopita  kwani alikuja mwenyewe kuifufua namba  yake”
 
Wakati tukiwa garini tukirudi kwa mzee Nasri, Amour aliniambia.
 
“Nina mashaka na madai kuwa Ummy alikufa”
 
“Kwa hiyo wazo la kuwa ni mzuka kama alivyoniambia yeye halina ukweli?”
 
“Mimi  kama polisi siwezi kukubaliana  na wazo  kama hilo”
 
“Pale kwao  wanasisitiza kuwa Ummy alishakufa na hata majirani niliowauliza wameniambia  kuwa Ummy alikufa kweli”
 
“Sasa kama Ummy alikufa kweli, yule aliyekwenda kuisajili ile namba ni nani?”
 
“Ndiyo  maana ninaliona wazo la huo mzuka linahitaji kufanyiwa kazi”
 
“Hivi  wewe unaamini kuwa mtu aliyekufa anaweza kuibuka  tena na kuwa mzuka?”
 
“lisemwalo lipo.  Ni vizuri jambo hili lichunguzwe”
 
Tulipofika  kwa mzee Nasri tulishuka kwenye gari. Mzee Nasri hakuwepo barazani. Amour akabisha  mlango wa nyumba yake.
 
Mzee Nasri akatoka.
 
“Karibuni” akatuambia.
 
Safari hii alitukaribisha sebuleni.
 
Baada ya kuketi Amour alimwambia.
 
“Tumekwenda katika  kampuni  ya simu tumeambiwa kuwa usajili wa ile namba ni wa mwanao Ummy”
 
“Inawezekana. Ile namba aliisajili yeye mwenyewe”
 
“Tuliambiwa aliisajili kwa mara ya kwanza miaka sita iliyopita. Baadaye alacha kuitumia kwa miaka mitano. Hivi karibuni alikwenda kuifufua kwa sababu namba yenyewe ilikuwa imefutwa”
 
“Alikwenda  kuifufua nani?” Mzee akauliza akiwa amemkazia  macho Inspekta Amour.
 
“Alikwenda kuifufua Ummy mwenyewe. Tumeoneshwa kitambbulisho  chake na siku hiyo hiyo alimppigia huyu kijana”
 
“Hilo jambo  haliwezekanai. Bado nasisitiza kuwa Ummy amekufa… Ummy amekufa…”
 
“Mzee huwezi kufufua namba ya mtu mwingine. Ni lazima uoneshe kitambulisho chako ili utambulike kuwa wewe ndiye mwenyewe”
 
Niliona jasho likimtoka yule mzee.
 
“Sijui niseme nini..!” akajisemea peke yake.
 
“Itabidi tulifukue kaburi la Ummy” Ispekata akamwambia.
 
Mzee akamkazia macho tena Inspekta.
 
“Kwanini?”
 
“Kwa sababu kuna madai kuwa Ummy hakufa. Na kama itathibitika  kuwa Ummy hakufa  anaweza kukabiliwa na kosa la jinai”
 
“Kama  italazimika kuwa  hivyo, mimi niko  tayari kuruhusu kaburi lake lifukuliwe ili mtibitishe kuwa  mwannangu alikufa”
 
Mzee akanitazama kwa kunilaani. Alikuwa kama  anayejiambia  mimi  ndiye niliyeyaleta yote yanayotokea.
 
Siku ya pili yake kikosi maalum cha polisi kikiongozwa na Inspekta Amour kilipewa kibali na mkuu wa polisi wa wilaya, cha kulifukua kaburi  la  Ummy kwa madai kuwa Ummy hakuwa amekufa.
 
Tulifika katika eneo  hilo la  makaburi saa nne asubuhi. Mzee Nasri na familia yake walikuwa wamesimama pembeni wakiangalia.  Uso wa Mzee Nasri ulikuwa umefadhaika. Kitendo  cha kufukuliwa  kaburi la  mwanawe kilikuwa kimemkera.
 
Mkewe na mdogo wake Ummy wallikuwa  na mawazo  tofauti. Wao walitaka kaburi hilo lifukuliwe ili wathibitishe ukweli wa mambo.
 
Kulikuwa na daktari kutoka hospitali ya  Muhimbili ambaye aliletwa kwa ajili ya kuuchunguza  mwili utakaopatikana ndani ya kaburi hilo.
 
Kazi ya kulifukua  kaburi hillo ilianza saa nee na dakika tano.
 
Kwa vile  wafukuaji  walikuwa polisi wawili, baada ya nusu saa tu kaburi hilo likawa wazi.
 
Makaburi ya kiislkamu yanakuwa na mfereji mwembamba unaolazwa mwili wa marehemu. Mfereji huo unaoitwa mwanandani hufinikwa na ubao wakati marehemu anapozikwa.
 
Ule ubao ulikuwa umeshaanza kuoza. Lakini sanda ya marehemu ilikuwa bado ipo ingawa ilikuwa imefubaa.
 
Polisi waliokuwa wamevaa mipira waliutoa mwili huo  na  kuuweka juu ya  kaburi kisha  wakaifungua ile  sanda upane wa kichwani.
 
ITAENDELEA kesho usikose Uhondo huu

No comments:

Post a Comment