Friday, May 19, 2017

KLABU YA WAANDISHI WA HABARI TANGA (TPC) YATOA MSAADA KWA WATOTO NJITI, BOMBO



Tanga, KLABU ya Waandishi wa habari Tanga imetoa msaada wa vitu mbalimbali kwa watoto Njiti hospitali ya Mkoa wa Bombo ikiwa ni kuwakumbuka.
Akizungumza mara baada ya makabidhiano, Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi Tanga, Hassan Hashim, amesema jamii imewasahau watoto hao hivyo kuwataka wakumbukwe.
Amesema msaada huo ni pamoja na sabuni, maziwa pamoja na Pempas na kuahidi kutoa msaada pale ambapo itakuwa ikihitajika.
Amesema Klabu hiyo imekuwa ikijikita katika mambo ya kijamii ikiwemo uchangiaji wa damu na kusaidia huduma za kjamii  wakati wa majanga.
Akitoa shukurani zake Kaimu Mganga Mfawidhi Mkoa, Goodkluck Mbwilo, amesema Klabu hiyo imefanya jambo la kuigwa na kusema kuwa kundi la watoto njiti limesahauliwa.
Amesema msaada huo utatumika kama ilivyokusudiwa hivyo kuwataka watu wengine wenye uwezo kutoa msaada kwa wakundi mbalimbali hospitalini hapo wakiwemo wazee na watoto.



Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Tanga (TPC) Hassan Hashim (kushoto) akimkabidhi Kaimu Mganga Mfawidhi Mkoa wa Tanga, Goodluck Mbwilo moja ya msaada wa maziwa, sabuni, pempasi na unga wa ulezi kwa  watoto njiti hospitali ya Mkoa wa Bombo Tanga jana. Nyuma ni manesi wa hospitali hiyo.


 Katibu wa Klabu ya Waandisi wa Habari Tanga (TPC), Anna Makange (kushoto) akimkabidhi mfuko wa pempasi Kaimu Mganga Mfawidhi Mkoa wa Tanga, Goodluck Mbwilo msaada uliotolewa na klabu hiyo kwa watoto njiti hospitali ya Bombo Tanga jana.

Mwanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari Tanga, Hadija Baghasha akimkabidhi chupa ya moto Kaimu Mganga Mfawidhi Mkoa wa Tanga, Goodluck Mbwilo ikiwa ni moja ya msaada kwa iliyotolewa na klabu hoyo kwa watoto njiti hospitali ya Rufaa ya Bombo jana

No comments:

Post a Comment