Tuesday, December 9, 2014

AJINYONGA BAADA YA KULAZIMISHWA KUOA MKE ASIEMTAKA

Kumekucha blog

Tanga,MKAZI wa kijiji cha Duga  Horohoro Tanga, Mbito Dilima amejinyoga hadi kufa  kwa kutumia chandarua chumbani kwake na kuacha ujumbe uliosomeka kulazimishwa kuoa mke usiemtaka haikubaliki.

Akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake, Kaimu kamanda wa polisi Mkoani Tanga, Juma Ndaki, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 2 usiku nyumbani kwao na  kuacha ujumbe uliosomeka kulazimishwa kuoa mke nisiemtaka sikubali.

Alisema uchunguzi  wa awali wa kipolisi umebaini kuwa marehemu alichukua uamuzi wa kujinyonga baada ya wazazi wake kumlazimisha kumuoa binti asiemtaka na kwa kipindi kiefu akilikataa na kuzusha mgogoro ndani ya familia.

“Uchunguzi wa awali wa kipolisi umebaini kuwa marehemu alijinyonga hadi kufa kwa kutumia chandarua chumbani kwake na kuacha ujumbe uliosomeka kulazimishwa kuoa mke nisiemtaka haikubaliki” alisema

“Ujumbe ule alikuwa ameuweka sikio la kulia kama wale wavuta sigara na ukiwa ameukunja----kwa sasa tunakamilisha uchunguzi na maiti tumeihifadhi hospitali ya Bombo” alisema Ndaki

Ndaki alisema polisi inaendelea na uchunguzi na inawahoji wazazi wa marehemu pamoja na majirani wakati wakiendelea na taratibu za mazishi na kutoa wito kwa wazazi kuwa na mahusiano mazuri kwa watoto wao kuepusha matukio mabaya.

Katika tukio jengine, Ndaki alilitaja kuwa Mfanyabiashara wa pikipiki (bodaboda), Juma Said alinusurika kuuwawa na watu  wanasadikiwa kuwa ni majambazi baada ya jaribio lao la kumteka kushindikana.

Alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 6 usiku maeneo ya Magomeni  Tanga baada ya watu hao waliokuwa watatu kupakia mishkaki na walipofika katika  eneo lenye mchanga mwingi walimuamuru kuachia pikipiki .

Alisema wakati wakibisha kwa maneno na kutishia kupigana mmoja wa majambazi hao alitoa sime na kumtaka aondoke zake vyengine watamkata mikono na miguu.

“ Wale majambazi walikuwa watatu na walitoka nae mjini na walikubaliana vizuri tu---walimpa elfu kumi na tano ili akubali kwani gharama yake kwa uhalisia ni elfu nne” alisema Ndaki

“Kila siku polisi imekuwa ikiwaeleza bodaboda kuwa na utaratibu wa kujiwekea muda wa kikomo cha kufanya kazi----wako na masikio yasiosikia dawa na matokeo yake ni kama haya” alisema Ndaki

Alitoa wito kwa madereva hao kuwa na umoja na kufanya mawasiliano katika vituo vyao hasa anapotokea mmoja wao kukodiwa nje ya mji hasa nyakati za usiku  ambazo zimekuwa zikitumiwa na watu wabaya.

                                          Mwisho

No comments:

Post a Comment