Monday, December 8, 2014

BENIN KWAWAKA MOTO

Watu 37 wauawa Beni, ADF-Nalu yanyooshewa kidole

Raia wa mji wa Beni wameanza kuukimbia mji huo kufuatia shambulio la waasi wa Uganda wa ADF-Naluusiku wa Jumamosi kuamkia Jumapili Desemba 7 mwaka 2014, shambulio ambalo limegharimu maisha ya watu zaidi ya 37.
Usiku wa Jumamosi Desemba 6 kuamkia Jumapili Desemba 7, watu wenye mapanga wanaoshukiwa kuwa waasi wa ADF-Nalu, kwa mujibu wa viongozi tawala , walishambulia vijiji 3 wilayani Beni mashariki mwa jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuwaua watu 37 na kumjeruhi mtu mmoja.
Kwa mujibu wa vyanzo vya RFI watu 37 waliuawa katika mashambulizi hayo, ambayo yanadaiwa kutekelezwa na waasi wa Uganda wa ADF-Nalu wanaoendesha harakati zao Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Mashirika ya kiraia mkoani Kivu Kaskazini yamesema kusononeshwa na mauaji hayo, ambayo yametimiza idadi ya watu 250 kuuawa wilayani Beni kwa kipindi cha miezi miwili. Watu zaidi ya 20,000 wameyahama makazi yao.

No comments:

Post a Comment