Tuesday, December 2, 2014

Kipenga Serikali za Mitaa Chapulizwa

Kumekucha blog

Tanga, CHAMA Cha Wananchi (CUF) Tanga kimezindua kampeni yake ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kuwataka viongozi wa dini kuacha kuikingia kifua CCM na badala yake wahubiri amani na utulivu vipindi vyote vya uchaguzi.

Akizungumza katika mkutano uliofanyika mtaa wa Ngamiani kati, Diwani wa Ngamiani Kusini, Mussa Mbarouk aliwataka viongozi hao kuwahubiria waumini wao amani na utulivu na kuacha kukishabikia cha cha Mapinduzi kwa madai kuwa kimeshindwa kuwaboreshea wananchi maisha yao.

Alisema chama cha CCM kimeshindwa kutekeleza ahadi zake  na kimekuwa kikiwakandamiza katika kodi mbalimbali zikiwemo za mapango na za biashara na hivyo kuwataka viongozi hao kuikumbusha Serikali hiyo ya CCM na kuacha kuikumbatia.

“Kuna baadhi ya viongozi wa madhehebu ya dini wamekuwa wakiikingia kifua chama cha mapinduzi kwa kudhani kuwa kitawasaidia katika mambo yao----ukweli ni kuwa imeshindwa kuboresha huduma na haina uwezo  zaidi ya kuwakandamiza” alisema Mussa

Alisema CUF itafanya kampeni mfululizo mjini na vijijini kueleza udhaifu wa CCM pamoja na ahadi ilizotoa ambazo hazijatekelezwa zikiwemo za kuwapatia huduma ya umeme na  maji safi vijijini

Alisema wananchi wa vijijini wamekuwa wakiishi katika mazingira magumu na wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita chama hicho kiliwaahidi kuwapelekea huduma ya maji safi lakini hakuna kilichofanyika.

Akizungumza katika ufunguzi huo, Diwani wa Ngamiani kati, Habib Mpa (CUF) aliwataka wananchi kukichagua chama hicho na kuacha kukichagua chama cha Mapinduzi kwa madai kuwa hakina jipya.

Alisema viongozi wa chama cha CCM wameshindwa kutetea maslahi ya wananchi na badala yake wamekuwa wakifanya kazi kwa mazoea na kushindwa kukanyana jambo ambalo limekuwa likiwagharimu wananchi.

“Musikichagua cha cha CCM kwani viongozi wake wamekuwa wakilindana hata mtu abainike kufanya ufisadi----hii imekuwa ikiwagharimu nyinyi wanyonge” alisema Mpa

Alisema hakuna tofauti ya mwananchi wa mjini wala vijijini na kila mtu analilia shida ambapo zamani maisha ya mjini yalikuwa nafuu na kila mtu alikuwa ikikimbilia na kwa sasa kilio cha maisha magumu ni kila kona.

Alisema maisha ya mjini yameelemewa na kodi nyingi na kuwalazimu baadhi ya wafanyabiashara kubadilisha aina ya biashara zao na hivyo kuwataka wananchi kuutumia mtaji huo kuwaondoa viongozi wa CCM walioshikilia nafasi za uongozi.

                                                       Mwisho 


No comments:

Post a Comment