Kumekucha blog
Tanga, JAMII ya Walemavu Tanga imetakiwa kujitokeza kwa wingi katika nafasi
za kugombea na kuitaka kuhakikisha
inawachagua viongozi ambao wataweza kutetea haki zao katika vyombo vya kutunga
sheria.
Akizungumza na watoto wenye ulemavu wa viungo wakati wa kutoa
zawadi za Krismass jana, Mratibu wa kituo cha walemavu Tanga (YDPC), Hendry
William, aliwataka walemavu kujitokeza
katika chaguzi za Serikali za mitaa zilizoanza kampeni zake juzi.
Aliwataka kuutumia vyema uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa
kujitokeza kwa wingi katika kugombea nafasi za kuongoza pamoja na kuwachagua
viongozi ambao watatetea maslahi yao.
“Leo ni siku ya furaha kuona kituo cha watoto wenye ulemavu
wa viungo wanazawadiwa zawadi ya Krismass wakiwa na wazazi na walezi wao---kupitia
hadhara hii nawaomba kuzitumia chaguzi za Serikali za mitaa kwa kujitokeza
kugombea” alisema na kuongeza
“Chaguzi hizi ni kipimo kwenu cha kuwatambua viongozi
wanaofaa--- hii ni pamoja na ninyi kujitokeza na kuwa wamoja kuhakikisha
munashika nafasi za kuongoza” alisema Hendry
Aliitaka jamii hiyo ya walemavu pamoja na ndugu na jamaa wa
watoto wenye ulemavu kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa
serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani na kuchagua viongozi wanaowapenda.
Akitoa nasaha zake wakati wa sherehe hiyo ya kuwagawia zawadi
za Krismass na mwaka mpya, Padri wa Kanisa la Magomeni, Ayoub Kuminambili,ameyataka
makampuni na taasisi za Serikali na watu binafsi kuweka kitengo maalumu cha
watu wenye ulemavu.
Alisema kufanya hivyo kutawawezesha jamii ya walemavu kuona
wanatambuliwa na hivyo mahitaji yao kushughulikiwa kwa haraka tofauti na sasa
ambapo taasisi nyingi hazina vitengo kwa walemavu na hivyo kuwa kero.
“Kupitia siku ya leo na waandishi wa habari tunayaomba
makapuni na taasisi za uma kuweka vitengo kwa walemavu---hii itawasaidia
kuharakisha kupatiwa huduma” alisema Kuminambili
Aliyakumbusha makambuni ya ujenzi wa majengo kukumbuka kuweka
miundombinu ya walemavu ikiwemo njia ili kuzifikia huduma na kumaliza
malalamiko ya walemavu kushindwa kufika kuliko na mahitaji.
No comments:
Post a Comment