Kumekucha blog
Tanga,WATU wawili wanaosadikiwa kuwa ni
majambazi wameuwawa na wananchi wenye hasira kali baada ya jaribio lao la
kutaka kupora fedha ofisi ndani ya kiwanda cha chokaa cha Meelkh Limited
kilichopo Amboni Tanga kushindikana.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu kamanda wa
polisi Mkoa wa Tanga, Juma Ndaki alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 3
asubuhi baada ya walinzi wa kiwanda hicho kurushiana risasi ndani ya kiwanda.
Akiwataja majambazi hao waliuwawa kuwa ni, Timoth Chales (36)
na Mwinyimkuu Hamis(46) wote wakiwa ni
wakazi wa Kinondoni Dar es Salaam na maiti zao kuhifadhiwa hospitali ya Rufaa
ya Bombo.
Kwa mujibu wa maelezo yake Ndaki, alisema majambazi watatu
walifanikiwa kutoroka kwa kuruka ukuta ambao ulikuwa umekuzungushiwa waya na
wananchi kushindwa kuwakamata baada ya kutokomea porini.
“Kukamatwa kwa majambazi hao haikuwa kazi nyepesi kwani
kulikuwa na kurushiana risasi zaidi ya nusu saa----kwa kushirikiana na wananchi
majambazi wawili waliwakamata” alisema Ndaki na kuongeza
“Baada ya majambazi watatu kutoroka wananchi wenye hasira
kali waliwashambulia kwa mawe na marungu na kufa wakati wakipelekwa hospitali
ya Bombo” alisema Ndaki
Ndaki alisema majambazi hao waliingia ndani ya kiwanda hicho
na kujitambulisha kwa walinzi kuwa wao ni wateja wa chokaa kutoka Dar es Salaam
hivyo kuomba kuonyeshwa ofisi ya mhasibu kwa kufanya malipo.
Alisema baada ya kufika kwa mhasibu majambazi hao
walimlazimisha kuonyeshwa sanduku la pesa na kumtishia kumkata shingo kama
hatoweza kutoa ushirikiano na kuzipata pesa hizo na kumtaka asipige kelele.
Alisema wakati majambazi hao wakiwa ndani mlinzi wa geti aliewaruhusu
kuingia ndani alipatwa na mashaka na ndipo alipowafuatilia nyendo zao na wakati
akiingia ndani alisikia kelele za mwizi na ndipo alipotoa taarifa kwa
wafanyakazi wa kiwanda hicho.
Alisema wafanyakazi na wananchi waliokuwa nje ya kiwanda hicho
waliingia ndani na kuanza kurushiana mawe na marungu na wajambazi watu
kufanikiwa kutoroka jambo lililowakasirisha na kuanza kuwapiga mfululizo.
“Polisi walipofika waliwachukua majambazi yale na wakati
wakiwa njiani kuelekea hospitali ya Bombo wote walishakufa----kipigo
walichokipata kilikuwa kikubwa kwani wote miili yao iliharibiwa vibaya” alisema
Ndaki
Akitoa wito kwa wananchi, kaimu kamanda huyo aliwataka kuacha
kujichukulia sheria mikononi na badala yake wavitaarifu vyombo vya usalama
kufanya kazi zake kwani kufanya hivyo amedai
kuwa ni makosa.
No comments:
Post a Comment