Tuesday, December 9, 2014

WAUMINI WAMKATAA MCHUNGAJI KANISANI

Hekaheka ya leo Desemba 09 inatoka Bukoba, inahusu Waumini kumkataa Mchungaji


Hekaheka ya leo Desemba 09 inatoka Bukoba, inahusu Waumini kumkataa Mchungaji

chruch-lane_1450480c
Kama hukusikiliza Hekaheka ya leo Jumanne ya Desemba 9 kupitia Clouds FM kwenye Leo Tena, inahusu Waumini wa Kanisa la TAG Bukoba kumkataa Mchungaji mpya aliyeletwa Kanisani hapo  kwa madai ya kumtaka Mchungaji aliyehamishwa na kupekwa sehemu nyingine arejeshwe.
Baada ya Waumini kumaliza Kuabudu kwa Nyimbo Mchungaji  huyo  Pius Alphonce aliinuka na kuanza  Kuhubiri ndipo baadhi ya Waumini walipoamka na kusema kuwa hawawezi kuendelea na Mahubiri kutokana na watu wachache wanaotaka kulivunja Kanisa hilo kwa maslahi yao binafsi, hivyo kutaka  Mchungaji wa zamani Erius Manoti aliyehamishiwa Karagwe arejeshwe.
Hali hiyo ilipelekea mahubiri hayo kusimama na kuzuka fujo na kusababisha ibada hiyo kuahirishwa.

No comments:

Post a Comment