Monday, April 27, 2015

BABA AMPA UJAUZITO BINTI YAKE

Pale ambapo baba na mwana wanaingia kwenye uhusiano bila kujua.. Baba Mwalimu, mtoto mwanafunzi !!

pregna
Kesi ya mzazi kuwa na uhusiano na mtoto wake wa kumzaa sio kitu kipya kukisikia.. hii haikuwa bahati mbaya, baba kaingia kwenye uhusiano na mtoto wake wa kike bila hata yeye mwenyewe kujua.. kilichofuatia ikawa ni ishu ya ujauzito.
Story imetokea Afrika Kusini, mwalimu mmoja amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kugundua kuwa msichana aliyempa ujauzito ni mtoto wake kabisa wa kumzaa.
Alfred Mokoena alianzisha uhusiano na mwanafunzi huyo mpaka akapata ujauzito bila kujua kuwa ni mtoto wake wa kumzaa.
Mokoena anasema hakujua kama mtoto huyo ni wa kwake, aliachana na mke wake wakati mtoto huyo akiwa bado  mdogo sana, hivyo malezi yote amekua kwa kulelewa na baba mwingine.
Hata hivyo binti huyo naye alisema hakuwa anafahamu kama huyo ni baba yake mzazi hadi walipokwenda kupima DNA na kinachomuumiza kwa sasa ni jinsi atakavyomwambia mwanae kwamba mzee huyo sio baba yake ila babu yake !!
Hautopitwa na stori yoyote inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment