Monday, April 27, 2015

IDADI YA VIFO LA AJALI YA TETEMEKO LA ARDHI NEPAL YAONGEZEKA

Idadi ya vifo vya watu iliyosababishwa na tetemeko la ardhi Nepal imeongezeka…

maafaJumamosi iliyopita kuliripotiwa kutokea kwa tetemeko kubwa la ardhi katika milima ya Everest huko Nepal ambapo si mbali na makazi ya watu.
Katika tukio hilo watu mbalimbali walifariki, mpaka jana Jumapili April 26 watu zaidi ya 2000 walikuwa tayari wamepoteza maisha huku majeruhi zaidi ya 5000 wakiripotiwa kuumia vibaya na kupelekwa katika hospitali mbalimbali.
maafa2
Habari iliyoripotiwa hivi punde inaeleza kuwa idadi ya vifo hivyo imeongezeja na kufikia 3, 351 na huenda idadi ikaongezeka wakati wowote kutokana na majeruhi kuwa katika hali mbaya.
Mamia ya watu ambao wanaishi karibu na milima wanadaiwa kuwa katika hali mbaya na kukosa mahali pa kuishi.
maafa3Athari zilizojitokeza bado nikubwa sana.. wapo watu wengi waliokosa makazi, wengine waliamua kulala kwa zaidi ya siku mbili nje kabisa huku wengine wakilala nje ya kwenye makazi ya muda yaliojengwa kwa mifuko ya plastiki.

No comments:

Post a Comment