Thursday, April 30, 2015

FLOYD MAYWEATHER ADAIWA KUMKACHA MANNY PACQUIAO, APATWA NA KITISHO

Eti itawezekana Floyd Mayweather amkimbie Manny Pacquiao ??

city

Floyd Mayweather ana jukumu la kuuthibitishia ulimwengu kwamba yeye bado ni mbabe ambaye hataki kupoteza pambano lolote kwenye ulingo.. Manny Pacquiao nae ana jukumu la kukaza msuli ili ahakikishe anatengua rekodi ya Mayweather.. watu wanahesabu saa kadhaa tu historia iandikwe pale MGM Grand Garden ArenaLas Vegas Marekani.
Siku moja tu kabla ya pambano hilo kufanyika, kocha wa Pacquiao, Freddie Roach ametamka kuwa huenda Maywether akagoma kupanda ulingoni siku ya pambano hilo kwa kuwa anahisi Floyd hakutaka pambano hilo liwepo ila wamamlazimisha.
floo
pac
Mabondia hao usiku wa jana walikutana na waandishi wa habari na kuonyesha mkanda ambao mshindi atakabidhiwa baada ya mchezo huo.
etiii
Kwa pamoja wamekutana na kila mtu ametoa ya moyoni, lakini kila mmoja kajigamba kushinda pambano hilo.. tusubiri tu hiyo kesho usiku kutakuwa na majibu gani ambayo dunia itayapata kutoka kwenye pambano.

No comments:

Post a Comment