Wednesday, April 22, 2015

HALI BADO NI TETE AFRIKA KUSINI

Mengine kutoka Afrika Kusini pamoja na picha 12 hali ilivyokua

South Africa immigrant attacks
Mitandaoni kumekuwa na picha na video nyingi zimesambaa zikionesha hali ilivyokuwa Afrika Kusini kwa zaidi ya wiki moja, tumesikia na kuona mashambulizi ambayo wamefanyiwa watu ambao sio raia wa Afrika Kusini ndani ya nchi hiyo, video nyingi na picha zinasikitisha.. watoto wanauawa, wanajeruhiwa.. vurugu ilikuwa kubwa sana.
South Africa immigrant attacks
Hapa ni ndani ya Kambi ya muda ambayo wamehifadhiwa wageni, yani walikuwa na maisha yao kawaida tu mtaani baadae wanajikuta ni wakimbizi.
Cha mwisho kilichonifikia ni kuhusu ishu ya Waziri wa Usalama wa South Africa, Nosiviwe Mpisa-Nqkula kutangaza kwamba sasa wanaoingia kupambana na watu wanaofanya vurugu hizo ni wanajeshi baada ya kuonekana kama Polisi wameelemewa nguvu na hali ilivyo mitaani, watu saba waliripotiwa kufariki pia.
South Africa immigrant attacks
Baadhi ya watu waliokusanyika kulaani mashambulizi ya wageni ndani ya Afrika Kusini.
South Africa immigrant attacks
Mtaani hali haikuwa sawa, hili ni sehemu ya kundi kubwa la watu waliokuwa wanaandamana kupinga Xenophobia, ubaguzi wa kutaka wageni waondoke Afrika Kusini.
South Africa immigrant attacks
Akina mama na watoto wao, wako kwenye foleni kusubiri chakula cha msaada ndani ya Kambi ya wakimbizi ambayo wamehifadhiwa kwa muda.
South Africa immigrant attacks
Waandamanaji wakiwa na silaha, hali haikuwa shwari hata kidogo kwa wageni.
South Africa immigrant attacks
Askari wakiendelea na zoezi la kuwakamata watu wanaochochea mashambulizi ya wageni
South Africa immigrant attacks
Mmoja ya majeruhi akipatiwa huduma ya dharura ya matibabu.
South Africa immigrant attacks
Hali ilivyo kwenye Kambi walizohifadhiwa wageni
South Africa immigrant attacks
Foleni ya kupokea chakula cha msaada ndani ya Kambi
South Africa immigrant attacks
Waandamanaji na silaha zao mtaani
South Africa immigrant attacks
South Africa immigrant attacks
Mfalme wa Wazulu, Goodwill Zwelithini. Analaumiwa kusababisha machafuko yaliyotokea Afrika Kusini kutokana na kauli yake aliyoisema kwamba wageni wanatakiwa warudi kwao. Jumatatu April 22 amekanusha kushinikiza machafuko hayo
Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe alisema kuna Watanzania waliouawa lakini mauaji hayo hayakutokana na vurugu hizi za kuwakataa wageni.
Pole kwa watu wetu wote ambao wameathirika kutokana na vurugu hizi.

No comments:

Post a Comment