Tuesday, April 28, 2015

KITISHO CHA UGAIDI YAIKUMBA BUNGE, KENYA

Kulikuwa na mpango wa shambulio la kigaidi Jengo la Bunge Kenya?? Mfanyakazi mmoja katajwa

Parliament_Buildings,_Nairobi,_Kenya_-entrance-15April2010
Kuna stori mpya kila siku kuhusu ishu ya ugaidi.. Kenya ni nchi ambayo imetajwa sana kukumbwa na mashambulizi ya kigaidi, kingine kilichoripotiwa ni kuhusu mmoja ya wafanyakazi wa Bunge kutajwa kushirikiana na Kundi la Al Shabaab kupanga kufanya mashambulizi katika Jengo la Bunge la nchi hiyo.
Ali Abdul Majid amekamatwa baada ya kupatikana kwa taarifa kwamba Al Shabaab wana mpango wa kushambulia baadhi ya maeneo ikiwemo Jengo la Bunge la Senate Nairobi.
Katika taarifa hiyo Al Shabaab walipanga kushirikiana na mmoja wa wafanyakazi katika Bunge hilo ambae anasali katika Msikiti wa Pumwani Riyadh, baada ya taarifa hizo Polisi walimkamata kwa ajili ya upelelezi.

Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment