Thursday, April 23, 2015

SOMA MAKUBWA YALIYOANDIKWA MAGAZETINI LEO APRIL 23 TZ

Uchambuzi huu wa magazetini unaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Elimu Cha Elimu Cha Candle Education Centre Tanga. Kituo kinaongoza kufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi cha sita wanaofanya mitihani ya Taifa na wale wanaojiendeleza kielimu. Kituo kimesajiliwa na NECTA. Wapo Tanga mkabala na Bank ya CRDB simu 0715 7727246

NYUUUUUUMWANANCHI
Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula ametumia kifungo cha vigogo sita wanaowania urais ndani ya chama hicho kuwatisha viongozi wa chini wasijihusishe na kampeni kabla ya muda kufika.
Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya kiongozi huyo kusema kuwa kanuni za uchaguzi za chama hicho zitawameza makada wake wanaotumia fedha kuwanunua wapigakura kama maandazi.
Akizungumza na viongozi wa chama hicho katika Jimbo la Kigamboni, wilayani Temeke, Mangula alisema: “Mnafahamu tulichokifanya kwa wanachama sita walioanza kampeni kabla ya wakati.”
Alisema kanuni za chama hicho zinaruhusu mwanachama kutangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi lakini haziruhusu kuanza kampeni kabla ya muda.
“Tuna ushahidi kwamba mmeanza kutoa vitu na fedha, nawaonya ndugu zangu acheni mambo hayo chama kina macho, kinawaona na kitachukua hatua,” alisema Mangula na kushangiliwa na viongozi wa chama hicho.
Alisema kamati ya maadili ya chama hicho iliwabana kwa maswali magumu makada walioanza kampeni kabla ya muda hadi wengi wao wakabaki midomo wazi.
Alisema walibaki midomo wazi kwa sababu waliwahoji huku wakiwaonyesha ushahidi wa makosa waliyoyafanya na shughuli walizozifanya.
“Kama watu hao maarufu tuliwapiga pingu kwa miezi 12 kwa kuanza kampeni kabla ya wakati, tutashindwa vipi kuwafungia nyie, tunafuata kanuni,” alisema Mangula.
Akifafanua namna Kamati ya Maadili anayoiongoza ilivyowabana kwa maswali viongozi hao, Mangula alisema; “tulipowaita mmojammoja tuliwaonyesha siku, tarehe na saa na fedha walizotoa wakati wakifanya kampeni kabla ya muda. Nadhani mnafahamu mtu mzima anapobainika kufanya jambo baya ni lazima anabaki mdomo wazi.”
Waliopata adhabu hiyo ni mawaziri wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Kilimo, Chakula na Kilimo, Stephen Wasira, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba na aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja.
MWANANCHI
Wakati viongozi wa CCM wanaendelea kupiga kelele bila ya kuchukua hatua dhidi ya vitendo vya rushwa wanavyodai vinafanywa na makada wanaotaka uongozi wa nchi, Takukuru iko tayari kukisaidia chama hicho kikongwe kupambana na uhalifu huo kama kitakuwa tayari kutoa ushirikiano.
Karibu viongozi wote wa CCM wameshanukuliwa wakilalamikia kukithiri kwa vitendo vya rushwa ndani ya chama hicho, hasa nyakati za uchaguzi, lakini wamekuwa wakieleza tu kwamba wahusika watawajibishwa na vyombo vya maadili vya chama hicho, licha ya vitendo hivyo kuwa vya uhalifu.
Juzi, akiwa kwenye vikao vya ndani na viongozi wa chama hicho wa Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Phillip Mangulla alisema fedha zinazotumiwa na makada kununua wanachama “kama maandazi”, zitakuwa kitanzi chao kwenye uchaguzi mkuu, akisisitiza kuwa wanachama hao watang’olewa.
Lakini wakati wasomi waliohojiwa na Mwananchi wanahoji sababu za chama hicho kutowashitaki makada hao kwenye chombo kinachojishughulisha na kupambana na rushwa, ofisa huyo wa Takukuru amesema inawawia vigumu wao kuwashughulikia wahalifu hao bila ya viongozi kutoa ushirikiano.
“Taasisi iko tayari hata kama viongozi au wanachama watatuletea malalamiko hayo leo (jana). Bila ushirikiano wa viongozi inakuwa vigumu kufuatilia,” Daniel Mtuka.
Kwa kesi ya rushwa kwa wagombea hao, ni vigumu kwani tuliwahi kukutana na changamoto ya kushindwa kufanya kazi yetu miaka iliyopita tulipomnasa mgombea fulani wa ubunge CCM ambaye pia alikuwa kiongozi wa chama. Sisi tulidhani ni tatizo, lakini hali hiyo ikaonekana kuwa siyo tatizo, akasema ni sahihi na ataingia kutekeleza ilani ya chama.
Alisema kutokana na mazingira hayo ni muhimu zaidi kupata ushirikiano wa chama ili kurahisisha kazi yao hasa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi ambacho kinatazamiwa kuwa na matukio mengi ya rushwa kuanzia ndani ya vyama vya siasa.
NIPASHE
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imeanzisha utaratibu mpya wa mafunzo kwa vitendo kwa watendaji wanaoandikisha wapigakura katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa kutumia mfumo wa Biometric Voters Registration (BVR).
Jumla ya BVR kits 498 zitatumika kutoa mafunzo hayo, lengo likiwa ni kurahisisha uandikishaji, baada ya awamu ya kwanza kusuasua katika Mkoa wa Njombe.
Mafunzo hayo yatafanyika kwa mikoa minne ya awamu ya tatu ya uandikishaji wapiga kura na yatakuwa endelevu ili kuharakisha uandikishaji utakaoanza Mei 2, mwaka huu.
Mkurugenzi wa Nec, Julius Malaba,  alisema Nec imeamua vifaa hivyo vitumike kwenye mafunzo ya vitendo kwa watumishi hao ili kuharakisha uandikishaji.
Awamu ya kwanza ya uandikishaji ilikuwa Mkoa wa Njombe, ya pili inayoanza kesho ni Mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Iringa na awamu ya tatu ni Dodoma, Mbeya, Katavi na Tabora.
Malaba alisema BVR 1,600 zilizowasili katikati ya Aprili, mwaka huu, zitatumika kuandikisha katika mikoa ya Iringa, Lindi, Mtwara na Ruvuma yenye watu wenye sifa ya kupiga kura ifikapo Oktoba, mwaka huu ni 2,599,205.
Tangu Februari 23, mwaka huu, Nec ilianza uandikishaji katika Mkoa wa Njombe wenye watu wenye sifa za kupiga kura 392,634, lakini hadi uandikishaji unafika Aprili 18, mwaka huu, walikuwa wameandikishwa watu 300,080 ikiwa ni tofauti ya watu 92,554.
Mkurugenzi huyo alisema BVR 1,600 zitakazowasili kati ya Jumamosi na Jumapili wiki hii, zitatumika kwenye awamu ya pili ya uandikishaji wapiga kura.
Alisema kwa sasa mafunzo kwa vitendo kwa idadi ya BVR zilizopo ni endelevu ili wakati wa uandikishaji kusiwe na ucheleweshaji kama ilivyotokea kwenye Mkoa wa Njombe kutokana na ugeni wa matumizi ya mashine hizo.
Aprili 2, mwaka huu, Mwenyekiti wa Nec, Jaji mstaafu Damian Lubuva, alitangaza kuahirishwa kwa Kura ya Maoni kwa Katiba inayopendekezwa kutokana na kushindwa kukamilika kwa daftari la kudumu la wapiga kura na itatangazwa tena.
Alisema tarehe ya kura hiyo itatangazwa tena baada ya Nec kushauriana na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec).
Nec ilisema hadi wakati huo, serikali ilikuwa imetoa Dola milioni 72 za Marekani sawa na Sh. bilioni 13.
Vifaa hivyo vinanunuliwa na serikali kupitia kampuni ya Lithotech Export ya Afrika Kusini ambayo imeingia mkataba na Nec na inaviagiza China.
Taarifa zilizopatikana ndani ya tume hiyo zinaeleza kuwa, kampuni hiyo ndiyo inayotoa muundo wa ndani (soft ware) ya mashine hizo na kwamba utengenezaji wa mashine moja na kuweka vifaa vyote muhimu inachukua wiki sita.
NIPASHE
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, ameanza ziara ya siku sita kwenye mikoa ya Tabora, Shinyanga, Mwanza na Kagera.
Ziara hiyo inalenga mwendelezo wa uzinduzi wa programu ya FTP maalum kwa ajili ya mafunzo ya uzalendo kwa vijana, shughuli ambayo amekuwa akiifanya tangu Januari mwaka huu.
Taarifa kwa vyombo vya habari jana iliyotolewa na Afisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene, ilisema ziara hiyo aliianza jana katika Wilaya ya Nzega, mkoani Tabora.
Alisema ziara hizo zitaambatana na mikutano ya hadhara wilayani Bariadi, Shinyanga kabla ya kwenda wilayani Ukerewe, mkoani Mwanza.
 Maeneo mengine atakayozindua programu hiyo ni Bukoba Mjini kisha Kyerwa na kwamba katika maeneo yote wamelialika Jeshi la Polisi kutoa elimu ya ulinzi shirikishi na polisi jamii.
Makene alisema pia, wameialika Taasisi ya Kupambana na kuzia Rushwa (Takukuru) ili kutoa elimu ya kupambana na kuzuia rushwa hasa wakati wa uchaguzi.
Aidha, alisema viongozi wengine wajuu wa chama hicho wataendelea na programu ya uzinduzi wa mafunzo ya kukiandaa chama kushinda dola na kuiongoza serikali, kwenye mikoa ya  Tanga, Shinyanga na Mbeya.
Alifafanua kuwa Makamu Mwenyekiti Taifa Bara, Prof. Abdallah Safari, atakuwa Korogwe Mjini na kuzindua mafunzo hayo kwa viongozi wa Korogwe mjini na vijijini kisha kufanya mkutano wa hadhara  Korogwe mjini.
Alisema, Naibu Katibu Mkuu Bara, John Mnyika, atazindua mafunzo wilayani Bariadi na pia atakuwa na mkutano wa hadhara Bariadi na Maswa.
Kadhalika, alisema Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, atazindua mafunzo hayo wilayani  Mbalizi na kufanya mkutano wa hadhara Njombe mjini.
MTANZANIA
Shilingi ya Tanzania imeporomoka kwa kasi katika miezi ya karibuni kiasi cha kutishia kuyumba kwa uchumi wan chi.
Katika takwimu za benki  kuu ya Tanzania BoT za Januari 2 mwaka huu, dola moja ya Marekani ilikuwa  ikiuzwa kwa wastani wa sh. 1586.
Mwishoni mwa mwaka jana dola ilifikia  sh. 1600 ingawa katika maduka  mbalimbali ya kubadilisha dola  moja ilikuwa ikinunuliwa kwa wastani wa sh. 18000.
Hata hivyo kwa siku za karibuni dola imepanda kwa kasi na hivi sasa inauzwa kwa wastani wa  1950 jambo ambalo limeongeza maradufu gharama ya bidhaa zinazoingizwa nchini  kutoka nje ambazo  hununuliwa  kwa dola za Marekani.
Pamoja na sababu nyingine zinazotajwa  kusababisha hali hiyo, hatua ya wahisani kugoma kutoa fedha  za misaada hususan ya bajeti inayofikia trilioni moja, inatajwa kuwa moja ya sababu  ya kuporomoka kwake.
MTANZANIA
Baba mzazi wa kiongozi wa ACT –wazalendo, Zuberi Kabwe, amesema pamoja na misukosuko ya kisiasa inayompaya motto wake, Mungu ndiye anayemsimamia.
Amesema kwamba kwa kuwa yeye ndiye mzazi wa mwanasiasa huyo amekuwa akimuombea mar azote, ikiwa ni pamoja na kipindi alichokuwa mwanachama wa CHADEMA.
“Mwanangu alibezwa na hata kuonekana kuwa si lolote katika chama  awali na kupewa majina mbalimbali, aliambiwa hata akitoka CHADEMA hatakuwa na athari zozote, lakini sasa kila Mtanzania  anashuhudia kinachoendelea”.
“ACT ni chama kidogo lakini  kinaongoza mitaa na vijiji na kimefanikiwa kuwa na wanachama wengi, sasa najiuliza hivi hawa waliokuwa wanasema  hana madhara, inakuwaje wanamkebehi Na hata kumuhofia?.
Anasema aliumia baada ya mwanaye kufukuzwa CHADEMA lakini sasa dunia yote inashuhudia hali halisi ilivyo kutokana na maono ya kijana wake.
Kila siku asubuhi na mapema tangakumekuchablog inakupa uchambuzi wa yote yaliyoandikwa magazetini, ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment