Monday, December 8, 2014

JE, UMEPITWA NA 255

Ulipitwa na 255 ya leo Desemba 8? Nimeirekodi na nimekuwekea hapa.


Ulipitwa na 255 ya leo Desemba 8? Nimeirekodi na nimekuwekea hapa.

3a90ebb1_IMG_5833
Kesi ya madai ambayo ilifunguliwa na mganga Sheikh Shariff dhidi msanii AT inatarajiwa kutolewa hukumu ijumaa hii ya tarehe 12 baada ya Mahakama kusikiliza pande zote mbili.
Kesi hiyo inahusu madai ya mganga huyo kwamba alimtibia msanii huyo pamoja na kumpandisha nyota lakini msanii huyo hakumlipa mpaka sasa.
Baada ya  Mtanzania Idris kushinda BBAHotshots 2014 siku ya jana imeonekana kama baadhi ya watu kutoka Afrika Magharibi, akiwemo msanii wa Nigeria Davido kupost ujumbe Twitter kuonesha kutoridhishwa na matokeo hayo japo muda mfupi baadaye aliufuta ujumbe huo lakini bado watu ambao hawakupendezwa waliendelea kumshambulia na wengine wakim-unfollow kwenye Twitter.
Diamond Platnumz ameshinda tuzo nyingine Nigeria ambapo tuzo hiyo haikuwa ya kupigiwa kura, ambapo ilikuwa inahusu msanii bora ambaye ameleta mabadiliko katika Sanaa Afrika.
Mastaa wengi walikuwa wakishiriki katika tuzo hizo ikiwa ni pamoja na mwanasoka Yaya Toure.
Sam Smith, Beyonce na Pharell Williams wametajwa kuwannia vipengele sita katika Tuzo za Grammy ambazo zitafanyika mwezi February mwaka 2015.
Uhusiano wa Chris Brown na Karrueche huenda ukarudi kutokana  na post ya Chris ambayo ameiweka mapema leo kwenye ukurasa wa Instagram amemuomba radhi Karrueche na kuonyesha kuwa yuko tayari kurudiana na mpenzi wake huyo

No comments:

Post a Comment