Monday, December 8, 2014

MSANII WA NYIMBO ZA INJILI AFUNIKA UZINDUZI WA ALBAM YAKE YA 2

Kumekucha blog

Tanga, WASANII nchini wametakiwa kuielimisha jamii kuishi kwa kuvumiliana na kusameheana kwa baadhi ya mambo hasa kipindi hiki cha uchaguzi wa Serikali za mitaa na kuelekea uchaguzi mkuu mwakani kupitia nyimbo zao.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa albamu ya pili ya  msanii wa nyimbo za Injili, Magreth Singano , Askofu Mkuu na Mwasisi wa Huduma ya Evangelism and Prayer Ministry of Tanzania (EPMT) Endrew Mhina alisema wasanii wako na nafasi kubwa kuielimisha jamii kupendana na kuishi maisha ya kiucha Mungu.

Alisema kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani wasanii wanatakiwa kutunga nyimbo ambazo zitaweza kuiunganisha jamii  kushirikiana katika mambo mbalimbali na kuondosha tofauti za kiimani.

“Kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuuu mwakani niwaombe wasanii kutunga nyimbo ambazo zitawaunganisha wananchi na kuondosha tofauti za kivyama” alisema

“Wasanii wako na nafasi kubwa ya  kuwaunganisha Watanzania na niwaombe kutunga nyimbo ambazo zitakuwa na faida kwa jamii---kuna baadhi wanashindwa kujitambua na kutunga ambazo hazina faida” alisema Mhina

Akizungumza kabla ya uzinduzi huo, msanii Magret Singano alikabidhi madawati 40 kwa shule ya msingi ya Masiwani kupunguza kero ya uhaba  kwa wanafunzi darasani.

Alisema mauzo ya albamu yake nusu atayapeleka katika kununua madawati na kuyapeleka katika shule ambazo wanafunzi wake wanasoma chini lengo likiwa ni kuisaidia Serikali katika jitihada zake za kuhakikisha shule zote wanafunzi wanakalia madawati.

“Kupitia kazi yangu ya kuimba nyimbo za Injili na kuguswa na elimu faida ya kazi yangu nitaipeleka katika elimu hasa upungufu wa madawati kwa baadhi ya shule” alisema Singano

Aliwataka wasanii wenzake na wadau wa elimu kuchangia madawati shuleni ili kuwawezesha watoto kuondokana na kero ya kusomea chini jambo ambalo linachangia kupata matokeo mabaya mwisho wa mwaka.

                                               Mwisho

Picha ya kwanza hadi ya tatu Askofu wa kanisa la Magomeni Tanga, Ayuob Kuminambili akiliombea box lenye CD za mwimbaji wa nyimbo za Injili, Magrert Singano kabla ya uzinduzi uliofanyika juzi.

Picha ya nne Askofu Mkuu na mwasisi wa Huduma ya Evangelism and Prayer Ministry of Tanzania (EPMT) akizindua CD za mwimbaji wa nyimbo za Injli iliyobeba jinala Furaha na Shangwe ambayo ni ya pili kuzindua.






No comments:

Post a Comment