Tuesday, April 7, 2015

SAFARI YA OBAMA KWENDA KWAO IKO PALE PALE

Safari ya Obama kwenda Kenya iko palepale.. Safari ya Miss World je?

Rolene Strauss
Hali ya nchi ikiwa sio nzuri kuna vingi vinaathirika, unaweza ukaona kwa haraka haraka tu kwamba athari kubwa ni vifo na uharibifu wa mali za watu.. lakini ukiiangalia kiundani athari yake ni kubbwa zaidi ya hapo.
Rolene Strauss ni mrembo wa South Africa ambaye alifanikiwa kushinda taji la Miss World 2014, leo ndio nimejua kwamba mrembo huyu alikuwa na ratiba ziara yake Nairobi Kenya na ilikuwa afanye hafls ya chakula cha usiku Nairobi March 10 2015 !!
Kutokana na ishu ya mashambulizi ambayo yametokea Chuo Kikuu cha Garissa Kenya, Rolene ameahirisha safari yake na amesema yeye pamoja na timu ya watu wake ilikuwa aje nao Kenya watatangaza tarehe nyingine ya kuja kwa ajili ya kuja Kenya.
Obama II
Kama hukujua ni kwamba mashambulizi ya Chuo hicho yamefanyika muda mfupi baada ya Rais Obama kutangaza kuwa atatembelea nchi hiyo July 2015.. hata baada ya mashambulizi kutokea bado amesema ratiba yake iko palepale.
Hutopitwa na habari yoyote inayonifikia na niko tayari kukupatia kupitia  www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment