 
          
      
MWANANCHI
Mgombea urais wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa, Edward Lowassa
 amesema kama Watanzania watashindwa kufanya mabadiliko kwa kupiga kura 
kuing’oa CCM madarakani mwaka huu, hawataweza kufanya hivyo tena, huku 
akihoji kama vyama tawala mbalimbali katika nchi za bara la Afrika 
vimeng’oka madarakani: “Kwa nini isiwe CCM”.
Lowassa aliyeambatana na Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye
 alisema vyama tawala vilivyokuwa rafiki na CCM vimeshang’oka madarakani
 na kwamba hivi sasa ni zamu ya chama hicho tawala kuondolewa.
“Nataka kura nyingi ili hata 
wakiiba tushinde, asilimia 90 ziwe zetu hizo 10 waache waibe. 
Msipoiondoa CCM mwaka huu hatutaiondoa tena, CCM na Tanu walikuwa na 
marafiki zao lakini karibu wote wameondoka.
“Chama cha Kanu cha nchini 
Kenya kimeshaondoka madarakani, kile cha Malawi (Malawi Congress Party) 
 nacho kimeondoka, UNIP (The United National Independence Party cha 
Zambia) nacho imeondoka na kile chama cha Mzee Obote (Dk Militon) cha 
Uganda kimeondoka, tunaona pia jinsi Rais wa Zimbabwe (Robert 
Mugabe) anavyohangaika,” Lowassa.
Katika mkutano huo, Lowassa alirudia vipaumbele vya ilani ya uchaguzi
 ya Ukawa, huku akimponda mgombea ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini kwa 
tiketi ya CCM, Frederick Mwakalebela kuwa hawezi kushinda kwa maelezo kuwa amepanda gari bovu.
Sumaye alieleza ufisadi mbalimbali uliotokea tangu Lowassa 
alipojiuzulu mwaka 2008, huku akihoji yalipo majina ya wauza dawa za 
kulevya na majangili ambayo alidai kwa nyakati tofauti Rais Jakaya 
Kikwete amenukuliwa akisema kuwa anayo.
Mkutano huo ulihudhuriwa na idadi kubwa ya wananchi ambao walianza 
kufika uwanjani saa nne asubuhi kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa huo. 
Baada ya kumalizika kwa mkutano huo saa 11.58 jioni, baadhi ya wananchi 
hao walilisukuma gari la Lowassa na mgombea ubunge wa Iringa Mjini kwa 
tiketi ya Chadema, Mchungaji Peter Msigwa hadi katikati
 ya mji huo kabla ya magari hayo kushika kasi na kuwaacha wakiendelea 
kukimbia barabarani huku wakiimba nyimbo mbalimbali.
Baadhi yao walionekana kubeba kitu mfano wa jeneza na kukivisha 
bendera ya CCM huku wakisema mwisho wa chama hicho tawala ni Oktoba 25.
Akiwa Mafinga Mjini, Lowassa alisema anahitaji Watanzania wampigie 
kura si chini ya milioni 10.2 ili awe rais na kumaliza kilio cha 
wakulima nchini.
Lowassa aliwaeleza wananchi wa Mafinga kuwa amechoshwa na manyanyaso 
ambayo wakulima wanaendelea kuyapata ikiwamo kukopwa mazao yao na 
kutozwa ushuru na Serikali bila ya wao kupata faida yoyote.
Lowassa alisema mara atakapochaguliwa kuongoza nchi, kitu kikubwa 
atakachokifanya kuwasaidia wakulima ni kufuta ushuru wote wa mazao na 
kuhakikisha wananufaika na jasho wanalolitoa wakati wa kilimo.
Sumaye aliwataka wananchi wa Mafinga kutokuwa na shaka na Ukawa kwa 
sababu wamejipanga vizuri kuhakikisha wanapata ushindi katika uchaguzi 
wa Oktoba 25, licha ya CCM kujipanga kupata ushindi wa goli la mkono.
“Tunawaomba Watanzania wachague
 Ukawa kwa sababu umefika muda wa mabadiliko, tunataka tupate wabunge 
300, hizo nafasi nyingine wagawane vyama vingine vilivyo nje ya Ukawa,”Sumaye.
Alisema Serikali ya sasa ni dhaifu kwa sababu wamekuwa wakipeana 
nafasi ya uongozi kindugu na ushikaji, hali inayofanya wananchi 
kuendelea kupata shida.
Katika mkutano huo, Waziri wa zamani, Joseph Mungai alipanda jukwaani kumnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, William Mungai ambaye ni mwanaye.
Waziri Mungai aliyewahi kuwa mbunge kwa miaka 35 kupitia CCM na 
alishika nafasi ya uwaziri katika wizara za Kilimo, Mambo ya Ndani na 
Elimu, alisema wananchi wa jimbo hilo wanatakiwa kumchagua William kwa 
sababu mbunge aliyemaliza muda wake hakuweza kuongoza kama alivyofanya 
yeye.
Alipoulizwa baadaye kuhusu nafasi yake kisiasa, Mungai alisema tangu 
aliposhtakiwa baada ya kura za maoni mwaka 2010, uanachama wake ndani ya
 CCM aliuweka kando na kadi yake hajawahi kuilipia.
“Kwa hivyo mimi ni mwanasiasa mstaafu, siko katika chama chochote,” alisema.
MWANANCHI
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa 
amesema amechoshwa na manyanyaso wanayoendelea kuyapata wakulima hapa 
nchi kwa kukopwa mazao yao na kutozwa ushuru na serilkali bila ya wao 
kupata faida yoyote.
Lowassa alisema punde atakapochaguliwa kuongaza nchi kitu kikubwa 
atakachokifanya kuwasaidia wakulima ni kufuta ushuru wote wa mazao 
kuhakikisha wakulima wananufaika na jasho wanalolitoa wakati wa kilimo.
Lowasa ameyasema hayo leo wilayani Mufindi alipofanya mkutano wa  
hadhara wa kampeni katika Uwanja wa Shule ya Msingi Wambi, mjini 
Mafinga.
Lowassa alisema watu wamekuwa wakizungumza kuwa CCM ni wezi wa kura 
kwasababu ni wajanja sana katika kufanya michezo michafu katika chaguzi 
na maneno hayo si yakuyabeza wala kuyafumbia macho.
“Mimi nataka kila mtu akihifazi
 vizuri kichinjio chake (kadi ya kupigia kura) na siku ya kupiga kura 
ikifika nawaomba wanawake na wanaume wajitokeze kwenda kupiga kura ila 
wakina baba nawaomba mkishapiga kura fanyeni kazi ya kuzilinda kura 
zenu” Lowassa
NIPASHE
Siku moja baada ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi 
(UKAWA) kuzindua kampeni zake wakati wakimtambulisha mgombea urais wao, Edward Lowassa, kwa kishindo jijini Dar es Salaam, mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, ameiponda ilani yao.
Dk. Magufuli amesema CCM ndicho chama chenye ilani inayoeleweka na 
imetaja mambo yanayogusa Watanzania, na siyo sawa na vyama vingine 
ambvyo havina ilani na vimeshindwa kuweka vipaumbele vyao.
Akihutubia mkutano wa kampeni wilayani Ludewa, mkoa wa  Njombe na Ruvuma, Dk. Magufuli alisema:
“Hadi sasa hakuna ilani ya Ukawa, leo mnawapa nchi watu ambao ni vyama vinne hadi sasa havijaweka ilani.”
Dk. Magufuli aliahidi kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Njombe
 hadi Ludewa, ambayo imeshafanyiwa upembuzi yakinifu na michoro kwa 
ajili ya ujenzi kuanza mwakani.
Mgombea huyo alisema serikali ya awamu ya tano itakuwa ya viwanda 
kila wilaya na kwamba itaboresha huduma za umeme, majisafi na salama, 
dawa mahospitalini, barabara za lami na wakulima kutokopwa mazao yao.
Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa jimbo la Ludewa mkoani
 Njombe na Madaba wa Ruvuma, alisema pia kila kijiji kitakopeshwa Sh. 
milioni 50 kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vijana na wanawake zikiwa ni 
jitihada za kujikwamua na umaskini.
Alisema pia serikali ya awamu ya tano itapunguza kama siyo kumaliza 
kabisa kero mbalimbali katika jamii kama waendesha pikipiki maarufu kama
 bodaboda kubughudhiwa na askari wa kikosi cha usalama barabarani na 
mama lishe kunyang’anywa mali zao.
“Serikali yangu itakuwa ya watu wanyonge, nitahakikisha huduma muhimi
 za jamii zinapatikana kwa wakati, mawaziri wangu watakuwa wa kuhudumia 
wanyonge,” alisema.
Alisema alipokuwa waziri alikuwa anaagizwa, lakini kwa sasa atagiza 
na akimwagiza waziri kupeleka maji sehemu fulani ni lazima afanye hivyo,
 vinginevyo atafutwa kazi haraka.
Kwa mujibu wa Dk. Magufuli,  kila awamu ya uongozi ina mambo yake na 
kufafanua kuwa  yaRais wa awamu ya kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, 
ilikuwa na kazi ya kuleta Uhuru na kuwaunganisha Watanzania na leo 
wamekuwa kitu kimoja.
Alisema awamu ya pili, tatu na nne zimeliwezesha Taifa kupiga hatua 
kubwa kimaendeleo na serikali yake ya awamu ya tano itakuwa ni ya 
mchakamchaka wa maendeleo kwa kuwa mazingira mazuri yalitengenezwa na 
watangulizi wake.
Aliahidi kuwa serikali yake itafanyakazi na vyama vyote, kwa kuwa 
hakuna anayezaliwa na chama isipokuwa kinachoangaliwa ni maendeleo na 
kwamba vyama si msingi wa maendeleo.
Alisema kazi kubwa itakayofanywa na serikali yake ni kuufuta umaskini na uchumi kumilikiwa na wanyonge.
NIPASHE
Mgombea udiwani wa Kata ya Bomang’ombe wilayani Hai kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Livingstone Nkya maarufu kama Ferefere, amefariki dunia ghafla muda mfupi baada ya kuzindua kampeni zake za kuwania nafasi hiyo.
Ferefere alifariki jana jioni baada ya kukimbizwa katika Hospitali ya
 Rufaa ya KCMC ya mjini Moshi, kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Katibu wa CCM Wilaya ya Hai, Allan Kingazi, alilithibitishia Nipashe 
kwa njia ya simu jana kuwa, mgombea huyo aliaga dunia baada ya kuzindua 
kampeni za uchaguzi kwenye kata hiyo.
Alisema Ferefere alianza kuhisi afya yake inabadilika na kumfanya 
kushindwa kuendelea na jukumu la kujieleza, hivyo aliamua kuondoka baada
 ya mkutano huo na kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Mkoa wa 
Kilimanjaro ya Mawenzi, kabla ya kuhamishiwa KCMC.
Kata ya Bomang’ombe ni miongoni mwa kata mpya tatu zilizogawanywa 
katika Jimbo la Hai, lililokuwa likiwakilishwa bungeni na Mwenyekiti wa 
Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe.
“Ni kweli mgombea wetu 
amefariki jana usiku katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC majira ya jioni; 
na hivi sasa tuko kwenye taratibu za kuandaa mazishi yake. Tunasubiri 
majibu ya daktari kujua amefariki dunia kutokana na tatizo gani, lakini 
sisi kama CCM tutasimamisha mgombea mwingine ili kutwaa kata hiyo,” Kingazi
Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Hai, Said Mderu alipotafutwa ili 
kutoa ufafanuzi iwapo uchaguzi huo utaahirishwa au laa, alisema,” Mimi sina taarifa za kifo hicho na kwa sasa nipo njiani, siwezi kuzungumza lolote. Nitafute kesho (leo) nitakuwa na majibu.
Ferefere ambaye pia ni mfanyabiashara maarufu wa maduka ya vileo na 
vinywaji baridi mjini hapa, alikuwa akigombea kiti hicho, akishindana na
 mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joe Nkya ambaye naye ni mfanyabiashara wa maduka ya pembejeo za kilimo.
NIPASHE
Aliyewahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati,
 amewapiga kijembe makada wanaohama CCM na kujiunga upinzani kuwa ni 
magamba yanayojivua yenyewe na kukiacha chama hicho kikiwa kisafi na 
kinachosimamia misingi yake ya kujali  wakulima na wafanyakazi.
Samia Suluhu Hassan, katika Jimbo la Manyoni 
Mashariki jana, Chiligati alisema CCM miaka ya nyuma iliwahi kuwataka 
makada waliokuwa na kashfa mbalimbali ambayo walipewa jina la magamba 
wajiondoe wenyewe na kwamba sasa ndiyo kazi hiyo imeanza kufanyika.
Chiligati ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Manyoni 
Mashariki na  ametangaza kustaafu siasa, alisema baada ya magamba hayo 
kujivua na kumalizika, CCM kitabaki kuwa cha wafanyakazi na wakulima 
kama kilivyokuwa tangu kinaasisiwa.
Alisema CCM kina wanachama zaidi ya milioni saba lakini kuna watu 
wachache wanakiharibia sifa yake nzuri na kuonekana kama chama cha 
mafisadi na kimetekwa na  watu wenye fedha nyingi.
Samia aliahidi kwamba ikiwa chama hicho kitashinda uchaguzi mkuu 
utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu, serikali yake itajenga kiwanda cha 
chokaa katika jimbo hilo ili kiweze kutoa ajira kwa vijana.
Pia aliahidi ujenzi wa barabara mbalimbali, kutatua matatizo ya maji 
na kulipa fidia wananchi ambao ardhi yao ilichukuliwa na serikali kwa 
shughuli mbalimbali bila kulipwa.
Samia aliahidi kwamba CCM kikishinda kitaendelea kujenga minara ya 
simu katika maeneo mbalimbali. Akiomba kura kwa wananchi, mgombea ubunge
 wa Jimbo la Manyoni (CCM), Yahaya Masare, alisema jimbo hilo lipo nyuma
 kimaendeleo lakini yeye amejipanga kutatua matatizo mbalimbali 
yanayowakabili wananchi.
Alisema shida ya maji katika jimbo hilo ni kubwa na kuwaahidi wananchi kwamba atashughulikia tatizo hilo ili kulimaliza.
HABARILEO
Aliyewahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati,
 amewapiga kijembe makada wanaohama CCM na kujiunga upinzani kuwa ni 
magamba yanayojivua yenyewe na kukiacha chama hicho kikiwa kisafi na 
kinachosimamia misingi yake ya kujali  wakulima na wafanyakazi.
Samia Suluhu Hassan, katika Jimbo la Manyoni 
Mashariki jana, Chiligati alisema CCM miaka ya nyuma iliwahi kuwataka 
makada waliokuwa na kashfa mbalimbali ambayo walipewa jina la magamba 
wajiondoe wenyewe na kwamba sasa ndiyo kazi hiyo imeanza kufanyika.
Chiligati ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Manyoni 
Mashariki na  ametangaza kustaafu siasa, alisema baada ya magamba hayo 
kujivua na kumalizika, CCM kitabaki kuwa cha wafanyakazi na wakulima 
kama kilivyokuwa tangu kinaasisiwa.
Alisema CCM kina wanachama zaidi ya milioni saba lakini kuna watu 
wachache wanakiharibia sifa yake nzuri na kuonekana kama chama cha 
mafisadi na kimetekwa na  watu wenye fedha nyingi.
Samia aliahidi kwamba ikiwa chama hicho kitashinda uchaguzi mkuu 
utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu, serikali yake itajenga kiwanda cha 
chokaa katika jimbo hilo ili kiweze kutoa ajira kwa vijana.
Pia aliahidi ujenzi wa barabara mbalimbali, kutatua matatizo ya maji 
na kulipa fidia wananchi ambao ardhi yao ilichukuliwa na serikali kwa 
shughuli mbalimbali bila kulipwa.
Akizungumzia tatizo la mawasiliano, Samia aliahidi kwamba CCM 
kikishinda kitaendelea kujenga minara ya simu katika maeneo mbalimbali.
HABARILEO
Chama cha ACT Wazalendo kimezindua kampeni zake jijini Dar es Salaam 
kwa kuahidi kitakapopewa ridhaa ya kuongoza nchi, kitaunda serikali ya 
Umoja wa Kitaifa.
Aidha katika uzinduzi huo ambao viongozi mbalimbali wa chama hicho walihutubia, Mgombea Urais wa chama hicho Anna Mghwira alisema wananchi wakimpa ridhaa, waziri mkuu wake atakuwa Zitto Kabwe.
“Nitakapounda serikali, katika 
katiba, mtu wa kwanza kusaidiana na rais licha ya makamu, ni Zitto 
Kabwe, atakuwa Waziri Mkuu katika serikali ya kwanza,” Anna Mghwira ambaye pia alisema atahusisha viongozi waadilifu kutoka CCM, Chadema na vyama vyote vya siasa na taasisi zote kiraia.
Akihutubia mkutano huo uliofanyika viwanja vya Mbagala Zakhem, 
mgombea huyo, katika kuelekeza nia yake ya kuunda serikali hiyo ya 
umoja, alisema linapokuja suala la kitaifa, hakuna haja ya kuangalia 
masuala ya itikadi. “Mimi ni mama, hukusanya watoto wake.
Hata mama wa vifaranga hukusanya vifaranga pamoja na kuviweka kwenye 
mbawa zake…mimi nina mbawa za moyo…nitaunda serikali ya umoja wa kitaifa
 itakayotokana na sekta binafsi lakini kutoka watu wazalendo, wenye utu,
 waadilifu, taasisi za kijamii, mashirika ya kidini, makundi ya umma ili
 kuunda taswira ya nchi yetu.”
Mghwira alisema taifa linahitaji mabadiliko si ya tu kifikra na 
kisera, bali pia ya kijinsia kwa kumchagua yeye kuwa Rais wa nchi. 
Alisema chama chake kinatilia mkazo utu, uzalendo na uadilifu.
Makao makuu Dodoma Aidha alisema, Serikali itakapoundwa itaapishwa 
Dodoma na watahakikisha wanarudisha kazi kubwa aliyoifanya Rais wa 
Kwanza, Julius Nyerere ya kuifanya Dodoma kuwa makao makuu ya nchi na 
serikali lakini siyo makao makuu ya chama.
Alisema kuweka mji huo makao makuu, maana yake ni kuleta watu wote 
kutoka pande zote za nchi. Vipaumbele Alitaja vipaumbele vyake ni kuwa 
na mfumo imara na endelevu wa hifadhi ya jamii unaojengea uwezo wananchi
 kukabiliana na majanga. Alisema asilimia sita pekee ya Watanzania 
wanafaidika.
“Tutatumia hifadhi ya jamii kama nyenzo ya kukuza akiba nchini ili 
kuwe na vyanzo vya mitaji ya uwekezaji wa ndani…tutapanua hifadhi ya 
jamii kufikia makundi yote katika jamii ikiwamo wakulima, wafugaji, mama
 lishe na bodaboda,” alisema. Kipaumbele kingine alichoahidi ni uchumi 
shirikishi wenye kuzalisha ajira nyingi na bora.
Alisema watu wengi hawana uhakika na maisha yao kimapato. Aidha 
alisema, watajikita kwenye uwekezaji wa kilimo na kusimamia uzalishaji 
wake. Aidha, aliahidi kuhakikisha ardhi na mashamba yote yaliyo chini ya
 mashirika ya umma, yanachukuliwa na kuwekwa chini ya uzalishaji mdogo.
Kwa upande wa viwanda, alisema atahakikisha bidhaa zinazozalishwa 
nchini zinaongeza mapato ya fedha za kigeni. Chama hicho kupitia kwa 
mgombea, kimesema kitaweka msukumo kwenye bidhaa za nguo na vitakuwapo 
viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ya kilimo na mifugo.
Vipaumbele vingine ni kuhakikisha madini, mafuta na gesi, vinakuwa 
mali ya wananchi kikatiba. Kuhusu Katiba Mpya, alisema wataruhusu Tume 
ya Jaji Warioba imalize kazi ya katiba ilikoishia. Mgombea huyo 
aliendelea kutaja vipambele vyake kuhakikisha anaboresha huduma za afya 
ikiwamo kudhibiti vifo vya mama na mtoto.
Aliahidi kuondoa tatizo la watoto wa mitaani. Misamaha ya kodi kwa 
mujibu wake, haitazidi asilimia moja ya pato la taifa na wakati huo huo 
atadhibiti mianya ya ukwepaji kodi hususani kwa kampuni za kigeni.
Sifa za rais Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitila Mkumbo,
 alishauri wananchi kuangalia wagombea urais kama wanalinda haki za 
walio wengi au ni mateka wa matajiri. Mkumbo alisema, kiongozi mkuu wa 
nchi, kwa maana ya rais, ana kazi kuu nne ambazo ni fikra na kutoa dira 
ya nchi jambo ambalo anapaswa kuwa na uwezo wa kufikiri.
“Tatizo ni kufikiri na kutoa dira ya nchi…tunataka rais atakayetoa 
misingi ya nchi, atatuletea sera..,” alisema Kitila. Alisema kazi ya 
pili ya rais, ni kuwa mlinzi mkuu wa tunu za taifa huku akisisitiza 
katika tunu ya umoja, wananchi kuepuka mgombea mwenye tabia za kidini, 
kikabila na kikanda.
“Rais ndiye mlinzi wa usawa katika taifa…,” alisema na kushauri 
wananchi kuangalia wanaogombea kama wanaelekea kulinda haki za walio 
wengi au ni mateka wa matajiri. Alitaja tunu nyingine ni muungano kwa 
kusema anayeomba urais na kutaka kucheza na muungano lazima akataliwe.
Kuhusu uadilifu, alisema inapaswa aingie rais atakayekoleza vita ya 
ufisadi . “Kama kuna mtu anataka urais hata kutamka neno ufisadi 
anaogopa, huyu hatufai hata kidogo,” alisema Kitila.
Akizungumzia demokrasia, alisema nchi imepiga hatua katika demokrasia
 ambayo inahitaji rais atakayeipeleka mbele. Vile vile alisema katika 
kuchagua, ni lazima kuangalia mgombea ndani ya chama chake 
alipatikanaje.
“Kazi nyingine ya rais lazima awe mfano wa binadamu bora katika 
jamii. Hatumaanishi malaika, tunamaanisha kwamba popote atakapoenda, 
akisimama wajue huyu ni Mtanzania, awe sura ya utaifa,” alisema na 
kusisitiza sifa nyingine ya rais itokane na uadilifu wa chama chake.
Kitila alisisitiza, “Mtu asiye mlaghai lazima aliyotuambia jana, na 
leo yafanane. Akihubiri maji lakini yeye anakunywa wiski, yeye ni 
mlaghai. Akituambia ni nyeusi jana, leo nyekundu, kesho nyeupe, huyo ni 
mlaghai.” Alisisitiza kuwa ACT Wazalendo inazingatia misingi na sera 
huku akibeza vyama vingine kwamba vinauza mbwembwe na ulaghai.
Ukawa wasutwa Kwa upande wake, Meneja wa Kampeni, Habib Mchange, 
aliisuta Chadema na CUF kupitia viongozi wao akirejea mkutano wa Mwembe 
Yanga mwaka 2007, walipotaja orodha ya waliowatuhumu kuwa mafisadi papa.
 “Kipindi kile hawakuwa na Ukawa bali walikuwa na ushirikiano.
Walitaja watu wanaofilisi taifa hili ambao ni watu kumi na moja…kati 
ya watu hao waliotajwa kuwa ni mafisadi, namba tisa alikuwa ni Lowassa,”
 alisema Mchange. “Tulikubaliana 2007 kwamba tunapambana na CCM na wana 
mafisadi. Leo naomba mtafakari…ili tusiwe wajanja wajanja lazima tuseme 
ukweli.
Unayosema jana ndo hayohayo uyaseme leo,” alisema. Akinyoshea CCM pia
 vidole, Mchange alilinganisha mgombea wa Ukawa sawa na chupa yenye sumu
 iliyobandikwa jina la maji. Alinadi chama chake akisisitiza wananchi 
wakiamini kwa kuwa kimekuja katikati ya sumu mbili za CCM na Ukawa.
Amshangaa Sumaye, Lowassa Mchange alisema anachoona ni kwamba, 
ufisadi uliokuwa CCM, umezaliana na kutanuka na hatimaye kuhamia Ukawa. 
“Jana (juzi) Sumaye ametulaghai… Anasema anashangaa kwa nini CCM 
inaendelea kuaminiwa,” alisema.
Alikumbusha kuhusu mjadala wa kununua ndege ya rais ambayo ilipigiwa 
kelele, kwamba wakati huo Sumaye ndiye alikuwa Waziri Mkuu. Pia kuhusu 
ahadi ya Lowassa ya kumwachia huru mwanamuziki Nguza Viking maarufu kama
 Babu Seya, Mchange alieleza kushangazwa naye kutokana na kile 
alichosema, wakati anafungwa, ndiye alikuwa Waziri Mkuu.
Mchange alikuwa mkali zaidi katika hotuba yake hasa alipokuwa 
anazungumzia ufisadi na wizi. “ Kumbe unaruhusiwa kuwaibia Watanzania 
ukiwa CCM ukirudi upinzani ni msafi. Mwizi ni mwizi tu.
Fisadi ni fisadi tu…Wanatudanganya kwamba kuna Ukawa…waongo. Ukawa 
wanatafuta rais tu. Ukawa huku chini kwa wapiga kura haupo,” alisema 
Mchange. Alihoji ni namna gani mgombea urais ataweza kunadi wagombea wa 
vyama vinavyounda Ukawa ambao wamegoma kuachiana majimbo hususani Jimbo 
la Tabora Mjini, Serengeti na Segerea.
“Sasa tuwaulize Ukawa Lowassa akipita Tabora mjini atamnadi nani?,” 
alisema akimaanisha mgombea wa CUF na Chadema wanaogombea jimbo hilo. 
Zitto Kabwe Alisema ACT Wazalendo wanarejesha miiko ya uongozi.
Alisisitiza kuhusu utaratibu wa chama chake wa kiongozi kutangaza 
mali na madeni yake. Zitto alisema kila chama kinachogombea, kinasema 
kitapambana na rushwa na ufisadi bila kueleza ni namna gani watapambana 
tofauti na ACT Wazalendo ambacho kimesema kitapambana kwa kurejesha 
miiko ya uongozi.
HABARILEO
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na Mbunge wa Urambo aliyemaliza muda wake, Samuel Sitta ametaka uandaliwe mdahalo kwenye vyombo vya habari kati yake na mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa uelezwe ukweli juu ya ukweli wa sakata la Richmond.
Sitta ambaye alikuwa Spika wa Bunge wakati Lowassa alipojiuzulu 
kutokana na sakata hilo, alisema katika mdahalo huo, ataeleza ukweli juu
 ya uhusika wa Lowassa katika sakata hilo na atatoa vielelezo kueleza 
taifa ufisadi uliokuwa ukifanyika.
Alisema hayo jana kwenye ufunguzi wa kampeni za CCM mkoa wa Shinyanga
 katika mkutano uliofanyika mjini hapa ambao wagombea wa udiwani na 
ubunge wa majimbo yote ya mkoani hapa walitambulishwa.
Katika mkutano huo, alisema kujiuzulu kwa Lowassa mwaka 2008, 
kulitokana na Kamati Teule iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe, 
kugundua kwamba fedha za walipa kodi zilikuwa zikipotea bure.
Alisema yuko tayari kusimulia kwa umma utajiri wa mgombea huyo wa 
Chadema. Makundi, urafiki Sitta ambaye ni Waziri wa Afrika Mashariki, 
ambaye pia alikuwa kwenye kinyang’anyiro cha kutaka kuteuliwa kugombea 
urais kupitia CCM, alisema wanamwamini Dk John Magufuli katika utendaji 
wake wa kazi na pia ni kiongozi asiye na makundi au urafiki.
“Kweli lazima uwapime viongozi,
 kwani anayetaka urais lazima achaguliwe kwa kufuata utaratibu, 
achambuliwe usiogope moshi kama unapikia kuni…lakini mwenzetu Lowassa 
hakukubaliana na hayo, akaona kaonewa kwa madai anafaa kuwa rais mbona 
sisi tulikubali?,”Sitta.
Aliendelea kusema, “hali hiyo, 
ilionesha ndani ya CCM kulikuwa na vyama viwili ambavyo ni ‘CCM Katiba’ 
na ‘CCM Maslahi’ ambayo alikuwa anaongoza Lowassa na mfuasi wake, Mgeja 
(aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga ambaye pia alihamia 
Chadema hivi karibuni).”
Wanachama mapandikizi Sitta alisema CCM ilikuwa imejaa wanachama 
walio mapandikizi tofauti na sasa ambapo alidai wamekwisha jionesha na 
kimekuwa chama kizuri kama ilivyokuwa enzi za hayati Baba wa Taifa, 
Mwalimu Julius Nyerere.
Alisisitiza kwamba kitazidi kuimarika na waliobaki wataendelea 
kutetea ilani na kuhakikisha chama kinaendelea kushika dola. Kwa mujibu 
wa Sitta, wakati wa mchakato, baada ya kumaliza vikao, Lowassa alikuwa 
akiitisha vikao vya kundi lake alilolibatiza CCM Maslahi na kuwaagiza 
wapambe wake kuitisha vyombo vya habari kushambulia watu ambao hawako 
kwenye mlengo wao.
HABARILEO
Mgombea Urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kupitia Chama Cha Demokrasia (CHADEMA) Edward Lowassa amesema kuwa endapo atafanikiwa kuwa Rais atahakikisha vituo vya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) vinakuwa vyuo vya ufundi Stadi.
Aliyasema hayo mjini Mafinga wilayani Mufindi mkoani Iringa jana 
wakati wa mkutano wa kampeni kupitia umoja huo na kusema kuwa mara 
vijana watakapotoka hapo watakuwa na uwezo wa kujiajiri.
Lowassa alisema kuwa kipaumbele chake kikubwa endapo atachaguliwa 
atakachopigania ni pamoja na elimu mbalimbali ikiwemo ya ufundi ambayo 
ni rahisi kwa kijana kupata ajira ikiwa ni pamoja na kujiajiri wao 
wenyewe.
“Umefika wakati sasa kwa 
kuwekeza kwenye sekta ya elimu hususani elimu ya ufundi ambayo 
itawasaidia vijana kukabiliana na wimbi la ukosefu wa ajira,” alisema Lowassa.
Aidha alisema kuwa elimu itagharimiwa na serikali kuanzia sekondari 
hadi chuo kikuu na anajua kuwa fedha za kuwasomesha wanafunzi kwa elimu 
za sekondari na chuo kikuu zipo.
Kwa upande wake aliyewahi kuwa Waziri Mkuu Frederick Sumaye alisema 
kuwa lengo kubwa la Ukawa ni kuhakikisha inapata majimbo mengi ya ubunge
 na udiwani ili waweze kuongoza halmashauri hapa nchini.
MTANZANIA
Mgombea urais wa Ukawa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Edward Lowassa, amesema anahitaji kura milioni 10.2  aweze kushinda uchaguzi mkuu.
Kutokana na hali hiyo amewataka Watanzania wajitokeze kwa wingi 
kupiga kura Oktoba 25 mwaka huu na   watakapomaliza kumpiga kura, wawe 
tayari kuzilinda   zisiibwe na Chama Cha Mapinduzi.
Lowassa aliyasema hayo mjini hapa jana alipohutubia maelfu ya wakazi wa Mji wa Iringa katika Uwanja wa Gangilonga.
“Mwaka huu ni lazima CCM waondoke madarakani kwa sababu vyama vikongwe vyote vyenye umri kama wa kwake vimeshaondoka.
“Angalieni Frelimo cha Msumbiji kimeshaondoka, kule Zambia nao chama 
chao kimeshaondoka, kile chama cha Obote (Milton Obote Rais wa zamani wa
 Uganda), kimeshaondoka, KANU cha Kenya nacho hakiko tena madarakani ila
 kimebaki ZANU P F cha Zimbabwe.
“Lakini kumbeni kwamba ili nishinde nahitaji kura milioni 10.2 na 
hizi zitapatikana tu kama mtajitokeza kupiga na kulinda kura zenu.
Kwa habari, matukio na ichezo ni hapahapa tangakumekuchablog