Friday, August 28, 2015

TOTTENHAM YAMSAJILI KINDA WA KIJERUMANI

Tottenham Hotspur wamsajili nyota huyu kutoka Ujerumani

Siku za kufungwa kwa dirisha la usajili Uingereza bado zinahesabika na kila klabu inajiandaa kufanya usajili wake wa mwisho kabla ya dirisha la usajili halijafungwa. Klabu ya Tottenham Hotspur ya Uingereza August 28 imetangaza kumsajili winga mshambuliaji.
2BBC119100000578-3213964-image-m-106_1440758254306
Spurs imefanikiwa kumsajili winga mshambuliaji aliyekuwa katika klabu ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani Son Heung-Min ambaye ni raia wa Korea Kusini kwa mkataba wa miaka 5 baada ya kumfanyia vipimo vya afya na kufuzu. Dau la pound milioni 21.9 lilitosha kuishawishi klabu ya Bayer Leverkusen kumuachia winga huyo.
2BBC112800000578-3213964-image-a-107_1440758261499
Tottenham Hotspur inamleta Son Heung-Min aliyeifungia Bayer Leverkusen magoli 21 katika mechi 58 za Bundesliga ili aje kushirikiana na Harry Kane ambaye ni mshambuliaji wa kati tegemeo kwa klabu ya Tottenham Hotspur.
2BBC115500000578-3213964-image-a-108_1440758268628
2BBC119F00000578-3213964-image-a-110_1440758280327
Kwa habari, matkuio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment