Thursday, August 27, 2015

BALOTELL ATOA KAULI TATU BAADA YA KUTUA MILAN

Hizi ni kauli tatu za Balotelli kuhusu Liverpool na masharti aliyopewa AC Milan

Mshambuliaji wa kimataifa wa Italia Mario Balotelli ambaye huwa ni kawaida kuwa katika headlines mbalimbali kutokana na tabia yake na matukio yake ambayo anafanya, August 27 kaongea sababu zilizomfanya asifanye vizuri akiwa Liverpool.
Mario BalotelliBalotelli alikuwa na maisha magumu Liverpool kwani msimu uliomalizika aliishia kucheza mechi 16 na kufunga goli moja pekee. Balotelli analaumi mbinu za kocha wa Liverpool Brendan Rodgers ndio zimemfanya ashindwe kufanya vizuri msimu uliopita.
“Lazima nikubali makosa yangu, mfumo uliyokuwa umechaguliwa na Rodgers haukuendana na mimi, wakati naanza nilikosa nafasi kadhaa za wazi, nilikuwa na nafasi chache za kufunga kwa bahati mbaya ukichanganya na majeruhi, sikulalamika niliheshimu maamuzi ya mwalimu na nilijiheshimu kama mchezaji professional”>>> Balotelli
Liverpool v West Bromwich Albion - Barclays Premier League...Football - Liverpool v West Bromwich Albion - Barclays Premier League - Anfield - 4/10/14 Liverpool's Mario Balotelli looks dejected Mandatory Credit: Action Images / Carl Recine Livepic EDITORIAL USE ONLY. No use with unauthorized audio, video, data, fixture lists, club/league logos or "live" services. Online in-match use limited to 45 images, no video emulation. No use in betting, games or single club/league/player publications. Please contact your account representative for further details.
“Tabia zangu sio tu kwa sababu nimekuja Milan hata wakati nipo Liverpool mfumo wa maisha yangu na tabia zangu zilikuwa kawaida, kwa mfano mwaka uliopita sikuwa na tatizo lolote katika maisha yangu binafsi zaidi ya kupiga picha nikiwa kwenye migahawa na kuweka Instagram lakini hiyo haikuwa na maana kuwa sikuwa nikifanya mazoezi lakini sikucheza”>>> Balotelli
Liverpool's Mario Balotelli (right) speaks with Liverpool's Daniel Sturridge and Liverpool's Jordan Henderson (centre) before taking the penalty during the UEFA Europa League match at Anfield, Liverpool. PRESS ASSOCIATION Photo. Picture date: Thursday February 19, 2015. See PA story SOCCER Liverpool. Photo credit should read: Martin Rickett/PA Wire.
“Nimeambiwa nibadilike nifuate mfumo wa Milan nitafanya hivyo bila tatizo lolote, nimekuwa na staili hii ya nywele kwa muda mrefu ila sitaendelea nayo tena, matatizo yangu hayakuwa ubora wangu ila tabia nimekuwa nikiambiwa maneno mengi sana”>>> Balotelli
Mario Balotelli amerudi AC Milan ya Italia ikiwa ni baada ya kuondoka msimu uliopita na kujiunga na Liverpool kwa ada ya uhamisho ya pound milioni 16 amerudi AC Milan akitokea Liverpool kwa mkopo wa muda mrefu.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment