Friday, August 21, 2015

MAAJABU NA KWELI

Unakaribishwa kucheki na hizi barabara zenye uwezo wa kuchaji gari linalotembea…

Roads UK
Teknolojia imefanikiwa kuleta mambo mapya karibu kwenye kila kitu, tumezoea kuona magari yanatumia petrol na diesel, yakagunduliwa magari yanayotumia gesi, sasahivi yapo mpaka yanayotumia umeme !!
Huenda kama una safari ndefu na gari lako linatumia umeme ukapata stress nyingine, kwa mfano gari likiisha chaji katikati ya safari inakuwaje??
Gari Umme II
Hiyo gari pia imechomewa kwenye Cable ya umeme inajaa chaji.
Teknolojia imefika pazuri, tunatambulishwa kwenye hizi barabara mpya, za kisasa kabisa ambazo kama unaendesha gari inayotumia umeme basi ukipita kwenye upande huo wa barabara gari inaendelea kuingiza chaji huku safari yako ikiendelea kwa amani zote kabisa !!
.
Hapa ni kwenye Kituo ambacho gari zimepaki kwa ajili ya kuchajiwa kwenye umeme.
Kwenye Jiji la Gumi, Korea Kusini kuna mabasi ya abiria ambayo yanatumia mfumo wa umeme, wao wameweka switch kwa ajili ya magari yanayotembea umbali wa kama Kilometa 25 wanakutana na cable za umeme kwa ajili ya kuchajia gari, hizo cable zimepitishwa chinichini na umeme wake.
Uingereza wako kwenye mipango kuweka hizo cable kila baada ya umbali wa kama Kilometa 32 hivi, ila mpango mkubwa zaidi walionao ni huu wa kuanza kutumia hizo barabara ambapo hakuna gari nyingine itaruhusiwa kupita upande huo wa barabara.
Gari UMEME ii
Kwenye hii picha unaona battery ikiwa low haina chaji inaonesha rangi nyekundu, ikiwa nusu chaji rangi ya njano na ikiwa full kwa rangi ya kijani.
Utaalam mwingi sana uko hapo aisee, unaambiwa gari haitasimama ili kuingiza chaji wala haitachomekwa cable za umeme.. chaji itaendelea kujaa kwenye gari kama inavyochaji simu kwa mfumo wa Wireless !!
Kuna sehemu tayari ndani ya Uingereza wamekamilisha ujenzi wa barabara hizo na majaribio yatafanyika muda si mrefu ndani ya mwaka huuhuu 2015… Unatamani hii ifike na Bongo mtu wangu?
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment