Wednesday, April 8, 2015

MAUAJI WA WATU WEUSI MAREKANI YAIBUKA UPYA

 Mauaji ya mtu mwingine mweusi Marekani

police-lineNi kama dunia ilianza kusahau matukio ya ubaguzi wa rangi, ishu ikarudi kuanza kuzungumziwa tena mwaka 2014 baada ya matukio ya watu wawili kuuawa mfululizo na Askari Marekani.
Leo hii ni story ya Afisa mwingine wa Polisi wa jimbo la CarolinaKusini kushtakiwa kwa mauaji, ushahidi wa video unaonesha Askari huyo alimpiga risasi nane mgongoni mtu ambae ni Mmarekani  mweusi.
Walter-Scott-2-600x313
Marehemu Walter Scott
Tukio hilo limetokea Jumamosi April 4 2015 ambapo shahidi mmoja alirekodi tukio hilo kwa video inayomuonesha Marehemu Walter Scott ambaye umri wake ni miaka 5o akikimbizwa na Afisa wa Polisi mzungu aliyekuwa na bunduki, akampiga risasi nane mgongoni, Walter alipoanguka alimfunga pingu.
screen-shot-2015-04-07-at-3-43-02-pm
Walter Scott akimkimbia Polisi
Afisa huyo Thomas Slager amejitetea kuwa Mmarekani huyo mweusi alikuwa akiendesha gari, alipomsimamisha kwa ajili ya kukaguliwa, alionekana kupingana na amri ya Polisi, akamuibia Polisi kifaa chake ambacho huwa Askari wanakitumia kuwapiga shoti ya umeme wahalifu, Askari huyo akaamua kumpiga risasi.
scw
Walter Scott akifungwa pingu na Polisi
Hata hivyo Thomas Slager ameshtakiwa kwa mauaji na anakabiliwa na adhabu ya kifo au kifungo cha miaka 30 jela.
ws_21d713ac97c0ce379d3b23a3adcae87d
Thomas Slager akipandishwa kizimbani

No comments:

Post a Comment