Wednesday, April 8, 2015

KONGAMANO LA VIONGOZI WA DINI KUZUNGUMZIA AMANI YA NCHI LAFANA TANGA



Tangakumekuchablog
Tanga, JAJI Mkuu mstaafu, Augostino Ramadhani, amewataka viongozi wa dini kuyatumia majukwaa yao kwa kuhubiri amani na kuvumiliana katika mambo ya dini hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2015.
Akizungumza katika warsha ya siku mbili ya mahusiano ya dini na amani ya nchi iliyofanyika mjini hapa leo, Augostino aliwataka viongozi hao kuwahubiria wafuasi wao kuvumiliana katika mambo ya dini kwani Watanzania utamaduni wao ni wa kuvumiliana.
Alisema kiongozi wa dini anaweza kuwa chanzo cha kuvurugika kwa amani ikiwa mahubiri yake atachanganya dini na siasa na hivyo kuwataka kuyatumilia majukwaa yao  kwa kuwahubiria amani.
Alisema kuelekea uchaguzi mkuu ni wajibu wa viongozi wa dini kuwataka wafuasi wao kushiriki katika uchaguzi  kikamilifu kwa kuchagua viongozi waoona wanafaa  bila ubaguzi wa rangi dini wala kabila.
“Nimefarijika kuwa mshiriki wa warsha hii kuzungumzia amani ya nchi kwani imekuja muda muafaka kuelekea uchaguzi mkuu mwaka huu tukiwa pamoja na viongozi wa dini mbalimbali” alisema Ramadhani na kuongeza
“Sote tunatambua kuwa viongozi wa dini wako na mchango mkubwa katika kuliweka Taifa letu katika misngi amani na kuvumiliana----huu ndio utamaduni wetu na ndio maana nchi yetu inasifika ulimwengini kote” alisema
Awali akifungua warsha hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Magalula, aliwataka viongozi hao wa dini kuwa mabalozi wazuri wa amani mara watakapomaliza mafunzo yao.
Alisema kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu viongozi wa dini wako na wajibu na haki ya kuwaelimisha wafuasi wao umuhimu wa kushiriki uchaguzi mkuu ujao.
Alisema kushiriki katika uchaguzi ni jambo muhimu kwani mpiga kura ataweza kumpata kiongozi anaemtaka na kuondosha manung’uniko kwa kuchaguliwa kiongozi ambaye hakumpenda.
“Ndugu zangu viongozi wa dini ni furaha yangu kuwa warsha hii itawajengea uwezo----ndugu zetu wourd vision wameona umuhimu wa kulifanya jambo hili kwa lengo tu la kudumisha amani ya nchi” alisema Mgalula
Alisema Wourd Vision imetambua umuhimu wa amani hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu na hivyo kuwataka kuyatumilia na kuwa mabalozi wazuri maeneo wanayotoka.
                                                    Mwisho

No comments:

Post a Comment