Friday, January 15, 2016

LUKUVI KUTUMBUA MAJIPU TANGA



Tangakumekuchablog
Tanga, WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi, William Lukuvi, amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza  kushughulikia kero za migogoro ya viwanja   na kumtaka kuwashughulikia vishoka wanauza viwanja zaidi ya mtu mmoja.
Alisema hayo leo wakati wa ziara yake Mkoani hapa kusikiliza kero za wananchi waliojazana ukumbi wa jengo la Mkuu wa Mkoa na kusema kuwa Tanga ndio kinara wa migogoro ya ardhi.
Alisema kwanza ni vyema kuwashughulikia maofisa Ardhi  ambao watabainika kuuza viwanja zaidi ya mtu mmoja sambamba na utoaji wa hati na kusema mwaka huu ndio mwisho wa migogoro ya ardhi.
“Mwaka huu ndio mwisho wa migogoro ya ardhi afisa ardhi yoyote ambaye atabaika kuuza kiwanja zaidi ya mtu mmoja tutamshughulikia na kumtafuta popote alipo hata kama mgogoro uko na zaidi ya mika ishirini” alisema Lukuvi na kuongeza
“Mwaka huu ni kutumbua majipu na matambazi na hata yake ambayo hayajaiva tutayaivisha ili tuyatumbue, Serikali ya Magufuli haitaki tena kusikia migogoro ya ardhi” alisema
Waziri huyo amemtaka Mkuu wa Mkoa, Mwantumu Mahiza kuhakikisha mashamba yanayomilikiwa na wawekezaji yanaendelezwa kwa matumizi bora ya ardhi pamoja na mashambapori .
Alisema kuna baadhi ya watu wamennunua mashamba kwa kisingizio cha uwekezaji badala yake wamekuwa hawayaendelezi na kuwazuia wananchi wenye uhitaji wa ardhi kuteseka.
Alimtaka kuunda kikosi kazi ambachio kitashirikiana na maofisa kutoka makao makuu kupitia majalada ili kuwabaini watu waliochukua ardhi kwa ajili ya uendelezaji na badala yake wamekuwa wakiyaweka ili kuja kuuza kwa faida miaka ijayo na kusema jambo hilo halikubaliki.
Akizungunmza katika kikao hicho , Mkuu wa Mkoa Mwantumu Mahiza alisema ameunda kamati ya kushughulikia migogoro ya ardhi ambayo iko ameiongezea wiki moja zaidi ili kutoa nafasi kwa wananchi kutoa malalamiko yao.
Alisema kamati hiyo imekuwa ikifanya kazi yake kwa kufika kila sehemu yenye mgogoro wa ardhi na mipaka na kutoa nafasi kwa wananchi kusema malalamiko yao kwa upana mkubwa.
‘Mheshimiwa Waziri tumeunda kamati ya kushughulikia malalamiko ya wananchi juu ya migogoro ya ardhi na mipaka na hivi nikuambiavyo tumeongeza tena wiki moja zaidi” alisema Mahiza
Mahiza aliwataka wananchi kutoa malalamiko yao kwa kamati hiyo na kusema kuwa atazifikisha kero zao kunakohusika na kupatiwa ufumbuzi na kuwataka kuwa watulivu wakati kero zao zinashughulikiwa.
                                            Mwisho




 Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo na Makaazi, William Lukuvi, akizungumza na wananchi kutoka kata mbalimbali ya jiji la Tanga waliofurika ndani ya ukumbi wa jengo la Mkuu wa Mkoa kusikiliza kero za migogoro ya Ardhi iliyoikumba Tanga.
 Waziri wa Ardhi, Nyumba Maendeleo na Makaazi, Wiliam Lukuvi, akipokea makaratasi ya malalamiko ya migogoro ya ardhi wakati wa ziara yake Tanga leo.
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makaazi, Wiliam Lukuvi akizungumza na wananchi waliofurika ukumbi wa jengo la Mkuu wa Mkoa wa Tanga kusikiliza kero za migogoro ya ardhi inayoikabili halmashauri ya jiji la Tanga leo. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza na watatu kushoto ni Katibu Tawala Mkoa, Salim Mohammed Chima.

  Diwani wa kata Maweni , Joseph Colvas (CCM), akitoa dukuduku lake  la malalamiko ya migogoro ya ardhi iliyokithiri ndani ya kata yake na kudai kuwa migogoro hiyo inalelewa na Idara ya Mipangomiji wakati wa ziara ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi , Wiiliam Lukuvi wakati wa ziara yake jana..

  Mkazi wa Masiwani halmashauri ya jiji la Tanga, Mwanaidi Liku, akilalamika kukithiri kwa migogoro ya Ardhi  Tanga na kusema kuwa migogoro hiyo imekuwa ikikua kila siku na kushindwa kupata ufumbuzi, malalamiko hayo aliyatoa jana wakati wa ziara ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi, Wlliam Lukuvi  leo



Mkazi wa Tanga, Frank Panis, akitoa malalamiko yake ya kiwanja wakati wa ziara ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi , William Lukuvi aliyoifanya leo Tanga.

No comments:

Post a Comment