Wednesday, January 6, 2016

MKUU WA MKOA WA TANGA ATEMBELEA VIWANDA




Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza akiangalia majani ya Chai ambayo tayari yameshatengenezwa kiwanda cha majani ya Chai wakati wa ziara yake ya kutembelea viwanda Mkoani humo ziara ambayo iko na lengo la kuhamasisha uzalishaji na ufufuaji wa viwanda vilivyokufa.


 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza,akipatiwa maelezo ya jinsi maziwa yanavyotayarishwa kuanzia kwa mfugaji mdogo hadi kiwandani   na  Afisa Uzalishaji maziwa  Tanga Fresh, Adam Mgamba wakati wa ziara ya kutembelea viwanda ikiwa na lengo la kuhamasisha  uzalishaji na ufufuaji wa viwanda vilivyokufa  ambapo Tanga ilikuwa Mkoa wa pili kwa viwanda.

  Afisa masoko kiwanda cha kutengeneza maziwa cha Army Diary, Hassan Shekue, akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza namna ambavyo maziwa ya Mtindi na Yogart yanavyotengenezwa wakati wa ziara yake ya kutembelea viwanda ikiwa na lengo la kuhamasisha uzalishaji na ufufuaji wa viwanda Mkoani ambapo Tanga ulikuwa Mkoa wa pili kwa viwanda.


Mtendaji Mkuu kiwanda cha kutengeneza mifuko cha (PPTL), Tarajit Singh (kulia) akimfahamisha  Mkuu wa Mkoa wa Tanga  Mwantumu Mahiza  (katikati) namna ya  mitambo inavyofanya kazi wakati wa ziara yake ya kutembelea viwanda Tanga  ziara ambayo iko na malengo ya kuhamasisha uzalishaji  ufufuaji wa viwanda vilivyokufa  Mkoani humo ambapo Tanga ulikuwa Mkoa wa pili kwa viwanda.

No comments:

Post a Comment