Saturday, January 16, 2016

WAUZA PEMBEMBEJEO ZA KILIMO WAILALAMIKIA SERIKALI , WATAKA USHURU UPUNGUE



Tangakumekuchablog
Tanga WAJASIRIAMALI sekta ya Ufugaji kuku, wakulima wa mahindi na  wauzaji wa pembejeo za kilimo Tanga wameiomba Serikali kupunguza kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ili kuwawezesha wakulima kumudu gharama na kulima kilimo cha kisasa .
Wakizungumza katika kongamano la Sekta ya Ufugaji kuku na wauzaji wa pembejeo za kilimo jana, lililoitishwa na BRAC kupitia mradi wa LEAD, walisema wajasiriamali  wengi  wadogowadogo wanashindwa kuiendeleza sekta hiyo  kutoka na gharama za pembejeo kuwa kubwa.
Walisema ni vyema Serikali ikapunguza ongezeko la Thamani (VAT) kwa pembejeo za kilimo na madawa lengo likiwa ni kuifanya kuwa kimbilio la watu wengi hata wenye kipato cha chini kuweza kumudu gharama za uendeshaji kilimo.
“Sekta ya kilimo na ufugaji imekuwa ikikimbiwa na watu wengi kutokana na gharama za pembejeo za kilimo, hii ni kutokana na kodi ya Serikali kuwa juu” alisema Ali Khatib Shunda
“Vijana wengi wako na dhamira ya kweli ya kujishughulisha na ufugaji na kilimo cha mahindi lakini wanashindwa kutokana ukubwa wa gharama za kodi za Serikali” alisema
Kwa upande wake Meneja wa mradi LEAD, Mohammed  Abdull Bari, alisema wafugaji wengi wanashindwa kubadilika kutoka kilimo cha mazoea na kwenda kwenye kilimo cha kisasa.
Alisema masoko yako mengi lakini wengi wa wafugaji na wakulima ni  waoga wa kuyafikia masoko yakiwemo ya ndani na la Afrika ya Mashariki  (EACT) ambapo wenzao wa jumuiya hiyo wanalichangamkia.
Alisema Shirika hilo la BRAC kupitia mradi wake wa  LEAD limekuwa likitoa elimu ya upatikanaji wa masoko  na kudai kuwa wengi ni waoga ilhali soko hilo la pamoja halina vikwazo.
“Kila tunapokutana nanyi tumekuwa tukitoa mbinu za kuyafikia masoko ndani na nje, kuna hili la jumuiya ya Afrika Mashariki naona wengi wamelala ilhali wenzao wanalichangamkia” alisema Bari
Aliwataka wakulima hao na wafugaji kuzidisha kasi ya miradi yao na kuwa wajasiri ya kutafuta masoko na kuacha kubweteka na masoko ya ndani kwani kutoka kwao kunaweza kuleta tija na mapinduzi ya miradi yao.
                                                Mwisho


Mfanyabiashara wa kuuza kuku soko la Ngamiani Tanga, Subeti Abdalla, akilalamika baadhi ya taasisi za fedha kuwakopesha na kuwatoza riba kubwa jambo ambalo linarudisha nyuma miradi yao na kushindwa kulipa kwa muda ukliowekwa wakati wa kongamano la Sekta ya ufugaji kuku

  Muuzaji wa pembejeo za kilimo Tanga, Giddo Mushi, akilalamika gharama za uagiziaji wa pemebejeo za kilimo kutoka nje na kuitaka Serikali kupunguza toza ya ushuru wa Thamani (VAT) ili kuwawezesha wakulima kulima kilimo cha kisasa na kuachana na kilimo cha mazoea.

No comments:

Post a Comment