Monday, December 12, 2016

JAPAN YATUMA CHOMBO ANGA ZA JUU KUZOA TAKA

Roketi ya H-IIB iliyobeba chombo cha Kounotori ikipaa angani baada ya kurushwa kutoka kituo cha anga za juu cha Tanegashima tarehe 9 Desemba
Japan imezindua chombo cha anga za juu ambacho kitabeba mtambo maalum wa kukusanya taka kutoka anga za juu.
Chombo hicho kitakuwa na nyaya ndefu za urefu wa mita 700 (nusu maili) ambazo zitatumiwa kuokota taka hizo. Nyaya hizo zitaundwa kwa madini ya aluminiamu na chuma cha pua.
Mtambo huo umeundwa kwa usaidizi kutoka kwa kampuni ya uvuvi.
Inakadiriwa kwamba kuna zaidi ya vipande 100 milioni vya taka kwenye mzingo wa dunia.
BBC

No comments:

Post a Comment