Sunday, December 11, 2016

WAITIMU MAHAFALI CHUO KIKUU OUT TAWI LA TANGA WAASWA


Tangakumekuchablog
Tanga, WAHITIMU Chuo Kikuu Huria (OUT) tawi la Tanga, wametakiwa kuwa mabalozi wazuri wa kupiga vita rushwa maofisini na  badala yake kuwa wabunifu katika utendaji kazi.
Akizungumza wakati wa mahafali ya 31 Chuo Kikuu Huria (OUT) tawi la Tanga jana, Katibu Tawala Mkoa wa Tanga, Zena Said, alisema kuna baadhi ya wakuu katika idara hawatoi huduma bila kudai rushwa.
Alisema tabia hiyo imekuwa ikirudisha nyuma maendeleo ya wananchi na kuamini kuwa huduma haitolewi bila kutoa rushwa jambo ambalo sio sahihi na kuwataka kwenda katika vituo vyao na kuwa mabalozi wema.
“Kupitia mahafali haya natambua kuwa hapa kuna wahitimu wa fani mbalimbali zinazogusa sekta nyeti ikiwemo ya polisi na utoaji wa huduma kwa jamii” alisema Zena na kuongeza
“Kuna dhana kwa baadhi ya watu kuamini kuwa huduma haitolewi bila kutoa rushwa, hii tunataka kuikomesha na kufanya hivyo ni ninyi hapa kuwa mfano kwa wengine” alisema
Kwa upande wao wahitimu wa mahafali hayo wameiomba Serikali kuongeza nafasi za ajira Serikali ili kuepuka elimu yao kuishia mifukoni.
Walisema kuna wimbi kubwa la watu wenye elimu lakini wamekosa nafasi za kazi hivyo kupunguza kasi ya ufanisi wa utoaji huduma kwa jamii na nguvu kazi ya maendeleo ya wananchi.
                                        




Mmoja wa wahitimu wa mahafali 31 Chuo Kikuu OUT tawi la Tanga akimuweka sawa mwanafunzi mwenzake kabla kwenda kutunukiwa cheti na mgeni rasmi Katibu Tawala Mkoa wa Tanga, Zena  Said juzi.

No comments:

Post a Comment