Sunday, December 11, 2016

LORI LA MAFUTA LALIPUKA NA KUUWA

Taarifa ya Lori la mafuta lililolipuka Kenya na kusababisha vifo

Lori la mafuta limelipuka nje ya mji wa Naivasha nchini Kenya usiku wa Jumamosi December 10 2016 na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 40.
Taarifa iliyotolewa mapema leo December 11 2016 asubuhi na msemaji wa idara ya taifa ya mambo ya dharura nchini Kenya Pius Masai amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kwamba magari zaidi ya 11 yameteketezwa kwa moto katika barabara ya Nairobi-Naivasha.
Maafisa kutoka wizara ya usafirishaji wakiongozwa na Katibu mkuu wa wizara hiyo Irungu Nyakera wamewasili katika eneo la tukio na Taarifa zaidi zinaeleza kuwa watu wengi wamejeruhiwa na miongoni mwao ni watu waliokuwa wakirejea nyumbani kutoka harusini subukia.
Katibu mkuu  Irungu amesema kuwa kwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa ajali hiyo imetokana na dereva kutokufahamu vizuri barabara hiyo kutokana na kwamba lori hilo la mafuta ni la nchini Uganda.
millardayo

No comments:

Post a Comment