Wednesday, December 14, 2016

WANANCHI WA KIJIJI CHA MAKINYUMBI WALALAMIKA KUTOSOMEWA MAPATO NA MATUMIZI



Tangakumekuchablog
Korogwe, WANANCHI kijiji cha Makinyumbi Miembeni kata ya Hale Wilayani Korogwe Mkoani Tanga wameutaka uongozi wa kijiji kuwasomea mapato na matumizi.
Wananchi hao wamedai zaidi ya miaka miwili hawajasomewa mapato na matumizi Ilhali  wako na  vyanzo vingi vya mapato ikiwemo minara ya simu na  mazao mashambani.
Wakizungumza kwenye mkutano wa wananchi kuzungumzia maendeleo ya kijiji, wananchi hao wamedai kuwa kwa kipindi kirefu hawajasomewa mapato na matumizi jambo linarudisha nyuma maendeleo ya kijiji.
Wamesema kufikia hatua hiyo watapeleka malalamiko yao kwa Waziri  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kutaka kutumwa wataalamu wa fedha kwa uchunguzi.
“Ni miaka miwili hatujasomewa mapato na matumizi nah ii inatia shaka kwani tunajua kuwa ukusanyaji ushuru wa mazao na kodi za wawekezaji zinaendelea kukusanywa” alisema Benantula Alphonce na kuongeza
“Kijiji chetu kiko nyuma kimaendeleo na huduma za kijamii na tumeshindwa hata kuweka zahanati angalau kuwaepushia kero wajawazito na wazee kufuata matibabu masafa marefu” alisema
Mwenyekiti wa kijiji hicho cha Mwakinyumbi  Miembeni, Erica Bahati, alisema hana hoja yoyote ya kujibu kero hizo kwa madai kuwa yeye sio msemaji wa kijiji.
Alisema hawezi kuzungumza na waandishi wa habari kwa vile hana taarifa za ujio wao na kibali cha kuingia kijijini hapo hivyo kuwataka kuwafuta waliowaita.
‘Mimi siwezi kuzungumza chochote kwani sio msemaji wa kijiji na pia ninyi mumefikaje hapa wakati hamna kibali na nani amewaita hadi kufika kwangu” alisema Bahati
Aliwataka waandishi hao pamoja na mwandishi wa habari hizi kufuata taratibu za kuchukua habari katika maeneo na kuweza kupata habari kwa kina ambazo zitasaidia kusukuma maendeleo ya wananchi.
                                       Mwisho


 Mkazi wa Korogwe Mkoani Tanga, Abdalla Jumanne, akitoa kero yake wakati mkutano wa wananchi uliofanyika jana kuzungumzia maendeleo na changamoto wanazokabiliana nazo.

  Mkazi wa kijiji cha Makinyumbi Miembeni kata  ya Hale Wilayani Korogwe Mkoani Tanga, Solomoni Hassan ju , akizungumza mbele ya wananchi wa kijiji hicho kuzungumzia kero mbalimbali wanazokabiliana nazo ikiwa na pmoja na kijiji kutosomewa mapato na matumizi.
Mkazi wa kijiji cha Makinyumba Miembeni kata ya  Hale Wilayani Korogwe Mkoani Tanga, Ester John, akitioa kero yake mbele ya wananchi wa kijiji hicho ikiwemo uhaba wa maji na kufuata matibabu masafa marefu.

No comments:

Post a Comment