Friday, December 16, 2016

HABARI NJEMA KWA WASHABIKI WA ARSENAL

Good news kwa mashabiki wa Arsenal kuhusu Danny Welbeck

Timu ya Arsenal ambayo katikati ya wiki hii ndio ilikuwa timu pekee ya Top 6 katika EPL kupoteza mchezo dhidi ya Everton Goodson Park kwa goli 2-1 na weekend hii watacheza na Man City, kocha wao ametoa good news kuhusu hali ya Danny Welbeck aliyekuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu.
Kabla hawajacheza mchezo dhidi Man City kocha wa Arsenal Arsene Wenger ametoa taarifa  kuhusu majeruhi ya Danny Welbeck ambaye alikuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu akiuguza jeraha lake la goti, Welbeck anatarajiwa kuungana na timu baada ya siku 7 hadi 10 zijazo.
screen-shot-2016-12-16-at-1-30-19-pm
Hivyo hiyo ni good news kwa mashabiki wa Arsenal kuhusu mchezaji huyo aliyekuwa akiuguza jeraha lake la goti toka mwezi May na ilitarajiwa kuwa inawezekana akawa nje ya uwanja kwa miezi 9, ila Wenger amethibitisha nyota huyo kuendelea vizuri na ataungana na wachezaji wenzake hivi karibuni.
millardayo

No comments:

Post a Comment