Monday, December 12, 2016

ARSENAL KUPEPETANA NA BAYERN MUNICH UEFA

UEFA: Arsenal v Bayern Munich; Man City v Monaco; Leicester v Sevilla

Arsenal wamepangwa kucheza na Bayern Munich, Leicester City watakutana na Sevilla nao Manchester City wakabiliane na Monaco katika hatua ya 16 bora Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Gunners wamecheza dhidi ya mabingwa hao wa Ujerumani mara nne katika misimu mitano iliyopita.
Walimaliza wa pili nyuma ya Bayern katika hatua ya makundi msimu uliopita.
Leicester City, mabingwa watetezi wa ligi kuu ya England, wana kibarua dhidi ya mabingwa watetezi wa ligi ndogo ya Ulaya, Europa League Sevilla ya Uhispania.
Wapinzani wa Manchester City Monaco walilaza Tottenham mara mbili katika Kundi E.
Droo kamili:
  • Manchester City (Uingereza) v Monaco (Ufaransa)
  • Real Madrid (Uhispania) v Napoli (Italia)
  • Benfica (Ureno) v Dortmund (GER)
  • Bayern (Ujerumani) v Arsenal (Uingereza)
  • Porto (Ureno) v Juventus (ITA)
  • Leverkusen (Ujerumani) v Atlético (Uhispania)
  • Paris (Ufaransa) v Barcelona (Uhispania)
  • Sevilla (Uhispania) v Leicester (Uingereza)

No comments:

Post a Comment