Saturday, December 10, 2016

ARSENAL YAJIKITA KILELENI

Arsenal Yaibamiza 3-1 Stoke City Na Kupaa Kileleni England


Mesut Ozil akishangilia baada ya kuifungia Arsenal bao la pili dakika ya 49 katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Stoke City kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Emirates, London. Mabao mengine ya Arsenal yalifungwa na Theo Walcott dakika ya 42 na Alex Iwobi dakika ya 75, wakati la Stoke lilifungwa na Charlie Adam dakika ya 29 kwa penalti baada ya Granit Xhaka kumchezea rafu Joe Allen kwenye boksi matokeo hayo yanaipandisha kileleni The Gunners kwa kufikisha pointi 34 sawa na Chelsea yenye mechi moja mkononi

No comments:

Post a Comment