Saturday, December 10, 2016

LIONS CLUB YATOA HUDUMA YA MACHO BURE HOSPITALI YA BOMBO TANGA



Daktari kutoka kituo cha Lions Club cha Mzizima Dar es Salaam, Shabbir Khanbhai, akimpima macho  mkazi wa Tanga, Mchumi Mbukuzi wakati wa zoezi la upimaji macho na utoaji miwani Bure pamoja na upasuaji zoezi lililofanyika jana hospitali ya Mkoa ya Bombo.
Zoezi hilo lilienda sambamba na upasuaji na utoaji wa miwani na dawa na kuwavutia mamia ya wakazi wa Tanga na nje ya Tanga ambapo Wataalamu wa mambo ya Macho wamedai kuwa kuna wimbi kubwa la watu wako na magonjwa ya macho lakini hawajitambui.
Mtaalamu huyo ambaye hakutaka kutaja jina lake kupitia kalamu ya tangakumekuchablog amedai kuwa kuna baadhi wamekata tamaa hasa kutokana na ugumu wa maisha na kuridhika na matokeo waliyonayo.




 Daktari kutoka kituo cha Lions Club cha Mzizima Dar es Salaam, Shabbir Khanbhai, akimpima macho mkazi wa Tanga, Tabu Pitter  wakati wa zoezi la upimaji macho na utoaji miwani na upasuaji zoezi lilifanyika jana hospitali ya Mkoa ya Bombo.



Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment