Tuesday, October 27, 2015

ARSENAL YALALA CAPITAL ONE

Sheffield Wednesday Vs Arsenal October 27 jana usiku na  matokeo ya mechi nyingine za Capital One

Usiku wa Jumatano ya October 27 kulikuwa hakuna mechi za Ligi Kuu Uingereza ila ilikuwa ni siku ambayo michezo ya ya Kombe la Capital One iliendelea nchini Uingereza kwa mechi kadhaa kupigwa katika viwanja mbalimbali Uingereza, moja kati ya mchezo wa Kombe hilo uliyochezwa ni Sheffield Wednesday walicheza dhidi ya Arsenal.
3384
Licha ya klabu ya Arsenal kuwa na mwenendo mzuri katika mechi za Ligi Kuu Uingereza msimu huu, haikufanikiwa kupata matokeo mazuri mbele ya Sheffield Wednesday, klabu ya Arsenal ilikubali kipigo cha goli 3-0, katika mchezo huo dhidi ya timu ya Sheffield Wednesday ambayo inashiriki Championship.
4928
Magoli ya Sheffield Wednesday yalifungwa na Ross Wallace dakika ya 28 ya mchezo kabla ya dakika ya 40 Lucas Joao kupachika goli la pili, goli ambalo lilidumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, kipindi cha pili kilianza kwa Arsenal kutafuta goli za kusawazisha ila Sam Hutchinson akaongeza goli la tatu dakika ya 52, goli ambalo liliwakatisha tamaa Arsenal ya kupata matokeo mazuri.
2610
Matokeo ya mechi nyingine za Capital One zilizochezwa usiku wa October 27
  • Everton 1 – 1 Norwich City (Mikwaju ya penati Everton 4 – 3 Norwich City)
  • Hull City 1 – 1 Leicester City (Mikwaju ya penati Hull City 5 – 4 Leicester City)
  • Stoke City 1 – 1 Chelsea (Mikwaju ya penati Stoke City 5 – 4 Chelsea)
3408
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment