Wednesday, October 21, 2015

MGOMBEA UBUNGE KATA YA MIKANJUNI AJITAPA



Tangakumekuchablog
Tanga,MGOMBEA Udiwani kata ya Mikanjuni halmashauri ya jiji la Tanga , Mwinyi  Kamari ( CCM), amesema endapo akichaguliwa kuwa Diwani ataondosha michango  isiyo ya lazima shule za msingi na sekondari.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara jana mtaa wa Madina, Kamari alisema kipindi chake cha Udiwani hatokubali kuona mwanafunzi amerejeshwa nyumbani kutokana na kushindwa kutoa michango.
Alisema watoto wote watasoma kama wengine na atanzisha mradi maalumu kwa wanafunzi wenye wazazi wenye kipato cha chini ili kuwawezesha kusoma hadi masomo ya juu.
“Ndugu zangu wananchi mtaa huu wa madina ambao mimi najiona kama niko nyumbani kwetu----nikiangalia nawaona wajomba mashangazi na wazee wangu ambao najua wote watanipa kura zao” alisema na kuongeza
“Sina shaka mwaka huu udiwani ni wa kamari ambaye ndie mwenye haiba na mvuto kwa wananchi kwa kunichagua kwa kura nyingi----nionavyo wala sina haja ya kupiga debe ila ni kupiga brashi “ alisema
Akizungumzia mazingira , Kamari alisema atachimba mifereji ya kupitisha maji katika mitaa ambayo nyakati za mvua inasababisha mafuriko kwa kuichimba na kuwa ya kudumu.
Alisema kuna baadhi ya maeneo ambayo nyakati za mvua hutuwama na hivyo kuwataka wananchi kuungana kwa pamoja ili kuweza kulimaliza tatizo hilo ambalo limekuwa likiwapa wakati mgumu wakati wa mvua za masika na za mwaka.
Alisema mifereji mingi imeziba kutokana na kutofanyiwa usafi hivyo akiwa Diwani atatoa ajira kwa watu ambao wataweza kuhudumia mifereji na kuweza kujipatia vipato vyao kupitia mifereji hiyo.
“Hakuana sababu ya vijana kwa wazee kukaa bila kazi -----ziko kazi nyingi na mimi nikiwa diwani nitanzisha miradi mbalimbali ikiwemo ya usafishaji mifereji” alisema Kamari
Aliwataka wananchi kumchagua ili kuwa Diwani wao ili kuweza kuibadili kata hiyo ambayo iko nyuma kimaendeleo ilhali iko na vyanzo vingi vya mapato na vijana kuweza kujiajiri.
                                               Mwisho

No comments:

Post a Comment