Thursday, October 22, 2015

JANJA YA MAMBA HII HAPA

Ukimwona Mamba kasinzia usidanganyike kabisa, hili ndio pozi lake la mtego !!


Mamba ni mmoja ya wanyama ambao kama ukikutana nao kwenye maji wana mabalaa yao, unaweza ukamchukulia kwamba sio mnyama mwenye mbio sana ukilinganisha na wanyawa wengine kama Simba na Chui, lakini ukimkuta kwenye maji balaa lake sio dogo !!
Wakati mwingine ni vizuri kujua tabia za wanyama ili kama kwa bahati mbaya ukikutana nae uwe unajua kabisa jinsi ya kuchukua tahadhari mapema.
Leo nimeipata hii ambayo sikuwahi kuijua siku za nyuma, Wataalam wa Australia wamekuja na majibu ambayo huenda ni watu wengi hawajui… kumbe Mamba anaweza kulala kwa kufunga jicho moja huku moja likiwa wazi…hilo ndio pozi lake la kujilinda na kuvizia pia wanyama ambao ndio chakula chake.
gettyimages-53343277-1-736x414
kingine ni kwamba Ubongo wa Mamba unaweza kulala nusu huku nusu ukibaki unafanya kazi sawa kabisa !! Kama na wewe ulikuwa huzijui hizo, basi nimekusogezea ili ikitokea unakutana na mamba amesinzia uwe na tahadhari yako kabisa hata kabla hujamsogelea.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment