Sunday, October 25, 2015

HAMASA UCHAGZU JIMBO LA MKINGA TANGA

 
Tangakumekuchablog
Mkinga, UCHAGUZI Wilayani Mkinga Mkoani Tanga, umekuwa wa kihistoria baada ya wananchi wengi kujitokeza katika vituo vya kupigia kura na kusababisha baadhi ya huduma muhimu ya usafiri wa magari yaendayo mjini na Wilayani pamoja na bodaboda kusitishwa.
Kabla ya kuanza kupiga kura mamia katika vituo vilikuwa vimefurika watu wakiwa wamejipanga  foleni kwa utulivu na mara maofisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuanza uchaguzi huo ulienda vizuri.
Kituo cha mabasi yaendayo mjini na vijijini vilikuwa vyeupe pamoja na maegesho ya pikipiki maarufu kama bodaboda pamoja na wafanyabiashara wenye maduka kufunga maduka yao ili kutekeleza haki yao ya kupiga kura.
Mkazi wa mtaa wa Mabatini Sokoni Maramba B, Juma Khamis, alisema alipanga kwenda Tanga mjini ili aweze kurudi na kuweza kupiga kura lakini alipofika kituo cha magari hakukuta gari hivyo kuahirisha.
“Nilipanga niende mjini kumuona ndugu yangu ambaye amelazwa  hospitali ili nirejee jioni kabla ya muda wa mwisho wa kupiga kura lakini sijakuta gari hata moja” alisema Khamis na kuongeza
“La kushangaza ni kuona hata bodaboda nao hawapo katika maegesho yao----inamaanisha nao wamenda kupiga kura na kuonyesha uchaguzi huu ni wa aina yake” alisema
Katika kata ya Mwakijembe, watu wengi walijitokeza kupiga kura na kuacha shughuli zao zote bila kujali jua kali ambalo lilikuwa linapiga huku baadhi ya wanawake wakiwa na watoto mgongoni.
Wanawake wengi wamejitokeza kupiga kura huku wakiwa na watoto wao migongoni na baadhi yao kupewa kipaumbele cha kuingia chumba cha kupigia kura pamoja na wazee na wagonjwa.
                                                Mwisho

No comments:

Post a Comment