Friday, October 23, 2015

MAGWI WA SOKA KURUDU DIMBANI

Hii ndio sababu iliofanya David Beckham, Ronaldinho, Ferdinand, Giggs, na mastaa wengine kurudi dimbani November 14…

Mastaa wa soka wa zamani watarudi dimbani kucheza katika mechi ya pamoja November 14 2015 katika dimba la Old Trafford. Miongoni mastaa wa zamani wa soka watakokuwepo katika kikosi cha timu hiyo ni David Beckham ambapo watacheza mchezo kwa ajili ya kuchangisha fedha katika mfuko wa UNICEF.
Beckham ambaye atakuwa nahodha wa kikosi hicho atajumuika pamoja na mastaa wenzake wa zamani kama Ryan GiggsPaul Scholes, Nicky Butt na Phil Neville na mastaa wote wa zamani wa Man United. Lakini upande wa timu ya David Beckham atajumuika na wachezaji wenzake wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza kama Rio Ferdinand, Sol Campbell, Ashley Cole, David Seaman na Jamie Carragher.
LISBON, PORTUGAL - JUNE 13:    Fussball: Euro 2004 in Portugal, Vorrunde / Gruppe B / Spiel 4, Lissabon; Frankreich - England ( FRA - ENG); Zinedine ZIDANE / ENG begruesst David BECKHAM / ENG . Links der deutsche Schiedsrichter Markus MERK 13.06.04.  (Photo by Andreas Rentz/Bongarts/Getty Images)
Mastaa wa zamani wa Man United mara ya mwisho kucheza mechi ya pamoja ilikuwa mwaka 2011 katika mechi kwa ajili ya heshima kwa Gary Neville. Lakini kwa timu pinzani itakuwa na mchezaji wa zamani wa Real Madrid kama Zinedine ZidaneRonaldinho, Luis Figo, Cafu, Fabio Cannavaro, Alessandro Nesta, Edwin van der Sar na Patrick Vieira, kwa upande wa Gary Neville bado hajathibitisha kama atakuwa sehemu ya mchezo huo.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment