Friday, October 30, 2015

JOSE MOURINHO AZIDI KUKALIA KUTI KAVU

Kwa mwenendo wa Chelsea vipi Jose Mourinho anafikiria watamaliza Top 4? hili ndio jibu lake…

Ikiwa masaa kadhaa yamesalia kabla ya klabu ya Chelsea ya Uingereza kucheza mechi na Liverpool katika uwanja wake wa nyumbani wa Stamford Bridge, huu utakuwa mchezo wa kumi na moja kwa Chelsea ambayo hadi sasa katika michezo kumi iliyocheza imefungwa mechi tano, imeshinda mechi tatu na kutoa sare mechi mbili na ipo nafasi ya 15 katika msimamo wa Ligi Kuu Uingereza.
Kocha wa klabu hiyo Jose Mourinho ambaye timu yake itacheza na Liverpool huku ikiwa na presha ya kutaka kuokoa kibarua cha kocha huyo ambaye anatajwa kama atapata matokeo mabovu katika mchezo huo, huenda akafukuzwa kazi, hata hivyo Mourinho ambaye ana maneno mengi ameshindwa kuthibitisha kuwa kama anaamini timu yake itamaliza katika nafasi nne za juu na kupata tiketi ya kucheza michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa msimu ujao.
2DF1F70E00000578-0-image-a-69_1446209906487
“Ni jinsi gani napambana na hii hali? ni kwa kufanya kazi sina mashaka tutatoka katika hiki kipindi kigumu mapema lakini siwezi kuahidi kuwa tutapata nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa msimu ujao, na kuhusu ulazima wa kushinda hii mechi, kwa kazi yangu huwa sishindi kila mechi ila huwa ni lazima kushinda kwa kila mchezo”>>> Jose Mourinho
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment