Friday, October 23, 2015

POLISI TANGA YAJIPANGA UCHAGUZI JUMAPILI



Tangakumekuchablog
Tanga, JESHI la Polisi Mkoani Tanga limesema limejiandaa kukabiliana na makundi ambayo yataonyesha kufanya fujo siku ya uchaguzi kesho na kuwataka wananchi kupiga kura na kuendelea na majukumu yao ya kujiletea maendeleo.
Akizungumz ana waandishi wa habari (leo) , kamanda wa polisi Mkoani Tanga, Zuberi Mombeji, aliwataka wananchi kupiga kura na kurejea maeneo yao ya kazi na kudai kuwa yoyote ambaye atakiuka sheria atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Alisema polisi itakuwa makini na kikundi au mtu yoyote ambaye atafanya fujo na hivyo kuwataka wananchi kutekeleza haki zao za kisheria za kupiga kura na kuwataka kufuata sheria.
“Ndugu waandishi wa habari kupitia kwenu naomba kuwaomba wanachi kutumia haki yao ya kuchagua kiongozi wanaemtaka kwa amani na utulivu kama uliopo----yoyote ambaye atakiuka sheria tutamchukulia sheria” alisema Mombeji na kuongeza
“Nendeni katika vituo vya kupigia kura na kasha rejeeni katika majukumu yaenu ya kujiletea maendeleo----musiwe na wasiwasi kama eti kutatokea fujo kwa kweli tumejipanga na kujidhatiti kwa atakaeleta fujo” alisema

Kamanda Mombeji aliwataka wananchi kuepuka mikusanyiko ya watu wengi kwani siku hiyo hawataruhusu mikusanyiko na hivyo kutakuwa na doria kila pembe na mitaa.
Alisema mikusanyiko yoyote polisi itaichukulia kama ni haramu hivyo ili kuweza kuepuka ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha anapiga kura na kwenda katika sehemu yake ya kazi ama kurejea majumbani.
                                        Mwisho


 Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga, Zuberi Mombeji akizungumz ana waandishi wa habari leo kuzungumzia juu ya usalama wananchi na mali zao ikiwa na pamoja na kusema kuwa jeshi hilo limejipanga kikamilifu kukabiliana na vurugu zozote ambazo zitatokea na hivyo kuwataka wananchi kupiga kura na kwenda katika shughuli zao za ujenzi wa Taifa






No comments:

Post a Comment