Friday, October 16, 2015

HASHIMU RUNGWE AJITAPA

Mgombea Urais kupitia CHAUMMA kayazungumza kuhusu kuanzishwa kwa chama chake pamoja idadi ya wabunge, madiwani…

Tukiwa bado kwenye headlines za Uchaguzi 2015 nakusogezea hii stori kutoka kwa mgombea Urais kupitia chama cha Ukombozi wa Umma, Hasheem Rungwe.

‘Chama cha Ukombozi wa Umma kilianzishwa mwaka 2012 lakini kilipata usajili 2013 mpaka leo hii kina uongozi wa kudumu na bahati nzuri mimi walinichagua kuwa mwenyekiti wa chama, malengo ya chama chetu ni kuwakomboa watanzania katika hali zao duni’- Hasheem Rungwe
‘Katika msafara wangu wa kampeni zangu nilikuwa na magari mawili katika mikoa mbalimbali na katika kampeni zangu nilikuwa napata watu walikuwa wanakuja na wananisikiliza mimi mgombea wa Urais wa Chama cha Ukombozi wa Umma’- Hasheem Rungwe
3 (1)
‘Idadi ya wadiwani na wabunge katika chama chetu kwanza sisi tumesimamisha wabunge katika mikoa isiyozidi 18 na katika mikoa hiyo yote tuna wabunge na tunao madiwani siwezi kukumbuka idadi yao lakini tunao madiwani Dar es Salaam tuna madiwani Temeke, tuna madiwani Kinondoni’ – Hasheem Rungwe
‘Cha mwisho ambacho ningependa kukisema ni kwamba wale wote waliopitishwa kugombea Urais wanye kwenye mdahalo wazungumzie na asije mtu kumsemea Fulani tunataka wagombea Urais tukutakane kwenye mdahalo ili wananchi wafahamu nini watakachoamua tarehe 25 Octoba, maana nimesikia kuna baadhi ya wagombea wanakwepa mdahalo, kwa hiyo mimi nataka mdahalo hata sasa hivi’- Hasheem Rungwe
hashim..2

No comments:

Post a Comment