Sunday, October 25, 2015

LOWASSA NAE APIGA KURA (MGOMBEA URAIS JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema anayeungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) Edward Lowassa amepiga kura, Monduli
Lowassa alipata nafasi ya kujibu maswali kadhaa ya waandishi ambao walitaka kujua kama atakuwa tayari kutakubali matokeo iwapo atashindwa.
Katika majibu yake, Lowassa amesema atakubali matokeo kama hayatachakachuliwa, vinginevyo hatakubali.
Waandishi pia walitaka maoni ya Lowassa kuhusu hukumu ya mahakama kukataza watu kukaa mita 200 baada ya kupiga kura.
Katika majibu yake, Lowassa amesema hali aliyoiona kituoni ni ya amani na utulivu hivyo hana maoni ya ziada kuhusu hukumu ya kukaa mita 200

No comments:

Post a Comment