Wednesday, October 28, 2015

COASTAL UNION YA TANGA YAENDELEA KUPEWA DOZI



Mshambuliaji Mganda wa Simba, Hamisi Kiiza amefunga bao pekee na kuipa Simba ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union.

Katika mechi hiyo iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, Simba ilipata bao lake katika dakika ya 8.

Bao hilo alilifunga baada ya kupokea pasi nzuri ya Hassan Kessy.

Hilo ni bao la sita kwa Kiiza raia wa Uganda ambaye alikosa mechi mbili za Simba kutokana na kuwa majeruhi.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment