Thursday, November 17, 2016

HADITHI, YAMENIKUTA SALMA MIE SEHEMU YA 31

HADITHI
 
YAMENIKUTA SALMA MIE
 
ILIPOISHIA
 
Alipotoka nilikwenda kumchungulia kwa dirishani nikamuona anaelekea kwenye kituo cha daladala. Nikaendelea kumtazama mpaka alipokata kona.
 
Bila shaka walishapigiana simu na Chinga tangu akiwa chumbani. Na alimwaambia kuwa nimemjibu jeuri ndipo akapanga safari ya kwenda kwa dada yake. Nikawaza.
 
Niliacha kufagia nikaenda chumbani na kuchukua simu yangu. Na mimi nikampigia Chinga. Nilipiga kwa muda mrefu lakini Chinga hakupokea simu yangu. Jambo hilo lilinihuzunisha sana. Ikabidi nijiulize tena iwapo kweli Chinga bado alikuwa na dhamiri ya kuendelea na mimi.
 
Kutokana na dukuduku lililonipata sikutoka tena kuendelea kufanya usafi wa nyumba. Nikajilaza kitandani na kuendelea kuwaza.
 
Sikutoka mle chumbani hadi ilipotimu saa sita mchana. Nilikwenda kuchukua soda kwenye friji nikanywa na keki nilizokuwa nimeziweka jikoni kisha nikaenda kuoga.
 
Niliporudi nilimpigia simu tena Chinga lakini sasa simu yake ikawa haipatikani.Nilizidi kuumia moyo wangu na kujuta kumkubali Chinga.
 
SASA ENDELEA
 
Nilikaaa mle chumbani hadi jioni nikimsubiri Chinga arudi ili nijue moja, lakini hadi inafika saa nne usiku si Chinga wala Vicky aliyetokea.
 
Kwa vile sikuwa nimekula mchana kutwa, nilitoka nikaenda kununua chipsi na mishikaki nikala na soda. Nilipomaliza kula nilifunga mlango na kwenda kulala.
 
Asubuhi kulipokucha niliona meseji ya Chinga kwenye simu yangu iliyosema.  “Usiwe mkali jifanye mjinga kwa akili yako. Nimeshakuambia nitakuhamishia Masaki”
 
Kwa sababu maji yalikuwa shingoni na sikuwa na la kufanya, yale maelezo ya Chinga yalinifariji kidogo ingawa nilijua Chinga hakuwa mtu wa kuaminika.
 
Nilitoka ukumbini ili niende msalani.Nikashituka nilipomuona Chinga amevaa taulo na Vicky aliyevaa khanga moja tu wakitoka chumbani na kuelekea sebuleni huku wakizungumza na kucheka.
 
Wamerudi saa ngapi? Nikajiuliza kwa mshangao.
 
Nikahisi bila shaka Chinga alirudi usiku wakati nikiwa nimelala.Akampitia mke wake huko kwa dada yake alikokwenda kisha wakaja pamoja.Kwa vile funguo alikuwa nayo, Chinga hakuwa na haja ya kunigongea mlango.Waliweza kufungua mlango na kuingia ndani bila mimi kujua.
 
Kile kitendo cha kuwakuta wamelala pamoja kilinichoma roho, nikajiona kama nimeshatemwa isipokuwa ninadanganywa tu.
 
Lakini nikajiambia nifuate vile Chinga alivyoniambia kuwa nijifanye mjinga kwa akili yangu ili nione mwisho utakuwa nini.Nikaenda msalani. Nilipotoka nikaanza kufanya usafi. Nilipofika sebuleni niliwasalimia kisha nikaendelea na usafi.
 
Nilipomaliza kazi hiyo Chinga alinituma vitafunio nikaenda kununua. Niliporudi niliandaa chai mezani. Chinga akaniambia tunywe pamoja, tukaenda kunywa na mke wake.Wenyewe walikuwa wanazungumza mimi nilikuwa kimywa.
 
Baada ya kunywa chai niliondoa vyombo nikaenda kuviosha. Nilipomaliza Chinga alinipa pesa niende sokoni. Niliporudi sokoni niliingia jikoni. Chinga na Vicky wakatoka. Sijui walikwenda wapi.Walirudi saa saba mchana wakati nilikuwa nimeshamaliza kupika
 
Nikataka kwenda kuwaandalia chakula lakini Chinga akaniambia wameshakula huko walikotoka na kwamba chakula nilichopika tutakula jioni.
 
Nikashukuru kwani kazi ya utumishi sikuipenda, nikaenda kula peka yangu.
 
Tulishinda salama hadi usiku. Baada ya kumaliza kula chakula cha usiku, rafiki zake Chinga walitokea.Chinga akamueleza mke wake kwamba wenzake wamemfuata kwa ajili ya safari ya kwenda Kibaha ambako walikuwa na shughuli zao.
 
“Utarudi saa ngapi?” Vicky akamuuliza.
 
“Kwenye saa saba au nane hivi”
 
“Sawa”
 
Chinga na rafiki zake wakatoka.
 
Ilipofika saa tano usiku mimi na Vicky tuliingia vyumbani kulala. Kama kawaida yangu nilikaa kitandani kwa muda mrefu bila kupata usingizi kutokana na kusongwa na mawazo.
 
Wakati usingizi unaninyemelea nilisikia mlango wa mbele unagongwa kwa kishindo. Nikatega masikio na kusikiliza. Mlango ukaendelea kugongwa.Nikainuka na kukaa kitandani.Niliposikia Vicky anafungua mlango wa chumbani mwao na mimi nilifungua mlango. 
 
 “Ni nani?” nikamuuliza.
 
“Ni John amenipigia simu, anasema amepigwa risasi ya bega” Vicky akanijibu.
 
Tukiwa tumeshituka tukaenda kufungua mlango.Tulimkuta John ameanguka chini kando ya mlango baada ya kuishiwa na nguvu. Mkono wake wa kulia alikuwa ameshika simu wakati bega lake la mkono wa kushoto lilikuwa linavuja damu ambayo iliunda mchirizi kuanzia alikotokea.
 
“Niingizeni ndani haraka!” akatuambia.
 
Wakati tunamshika ili tumuingize ndani tukasikia mbwa anabweka. Kutupa macho tuliona polisi wanne mmoja amemshikila mbwa aliyekuwa akiwaongoza kufuatilia ile njia aliyokuwa ameipita Chinga. Nyuma ya polisi hao kulikuwa na gari ya polisi inayowafuata.
 
Kutokana na mwanga wa taa iliyokuwa inawaka mbele ya nyumba yetu, polisi hao walituona. Nikamuona Chinga akiachia simu na kutia mkono ndani ya shati lake akatoa bastola aliyompa mke wake. 
 
“Ficha hii bastola!” akamwaambia.
 
Vile Vicky anaipokea tu bastola hiyo, sauti ya mmoja wa polisi hao ikatuamuru.
 
“Nyote mikono juu, mko chini ya ulinzi!”
 
Polisi hao walikuwa wameshafika karibu na mbwa aliyekuwa akimbwekea Chinga aliyekuwa amelala chini. Polisi wawili miongoni mwao walikuwa wametuelekezea bunduki.
 
Vicky alibaki na bastola aliyopewa na Chinga akiwa hajui la kufanya. Mimi niliinua mikono juu huku nikitetemeka. Sikujua nini kilikuwa kimetokea.
 
“Nyinyi wanawake ndiyo mnaofuga majambazi!” mmoja wa polisi hao akatuambia.
 
“Nani jambazi!” nilithubutu kumuuliza.
 
Hapo ndipo tulipoelezwa na polisi hao kwamba Chinga alikuwa jambazi na kwamba yeye na wenzake watatu walikwenda kuvunja duka moja pale Sinza lakini tayari walikuwa wamewekewa mtego na polisi. Wakavamiwa na kuanza kutupiana risasi na polisi. Chinga akapigwa risasi ya bega na kukimbia. Wenzake wawili waliuawa na mmoja alikimbia na gari walilokuwa nalo.
 
Lo! Sikujua,kumbe Chinga ni jambazi? Nikawaza.
 
Ni kwa sababu tu ya tamaa yangu ya kupenda pesa sasa nimejiingiza katika matatizo yasiyonihusu na nisiyo yajua.
 
Wakati tunamshika ili tumuingize ndani tukasikia mbwa anabweka. Kutupa macho tuliona polisi wanne mmoja amemshikila mbwa aliyekuwa akiwaongoza kufuatilia ile njia aliyokuwa ameipita Chinga.Nyuma ya polisi hao kulikuwa na gari ya polisi inayowafuata.
 
Kutokana na mwanga wa taa iliyokuwa inawaka mbele ya nyumba yetu,polisi hao walituona. Nikamuona Chinga akiachia simu na kutia mkono ndani ya shati lake akatoa bastola aliyompa mke wake.  “Ficha hii bastola!” akamwaambia.
 
 
Polisi hao walikuwa wameshafika karibu na mbwa aliyekuwa akimbwekea Chinga aliyekuwa amelala chini.Polisi wawili miongoni mwao walikuwa wametuelekezea bunduki.
 
Vicky alibaki na bastola aliyopewa na Chinga akiwa hajui la kufanya. Mimi niliinua mikono juu huku nikitetemeka. Sikujua nini nilikuwa kimetokea.
 
“Nyinyi wanawake ndiyo mnaofuga majambazi!” mmoja wa polisi hao akatuambia.
 
“Nani jambazi!” nilithubutu kumuuliza.
 
Hapo ndipo tulipoelezwa na polisi hao kwamba Chinga alikuwa jambazi na kwamba yeye na wenzake watatu walikwenda kuvunja duka moja pale Sinza lakini tayari walikuwa wamewekewa mtego na polisi. Wakavamiwa na kuanza kutupiana risasi na polisi. Chinga akapigwa risasi ya bega na kukimbia.Wenzake wawili waliuawa na mmoja alikimbia na gari walilokuwa nalo.
 
Lo! Sikujua,kumbe Chinga ni jambazi? Nikawaza.
 
Ni kwa sababu tu ya tamaa yangu ya kupenda pesa sasa nimejiingiza katika matatizo yasiyonihusu na nisiyo yajua.
 
Baada ya polisi kutupa maelezo yaliyoonyesha kuwa Chinga    alikuwa ni jambazi na alipigwa risasi wakati yeye na wenzazke    walipojaribu kuwashambulia polisi, Chinga alibebwa juu juu na kupakiwa ndani ya gari ya polisi.
 
Vicky aliyekutwa na ille bastola mkononi aliulizwa alikuwa akihusianaje na Chinga, akajibu kuwa alikuwa  mume wake.Yeye naye akakamatwa..Mimi nilipoulizwa nilieleza kuwa nilikuwa mtumishi wa ndani. Jibu hilo ndilo lililonisalimisha nikaachwa nibaki na nyumba.Lakini nilitakiwa kufika kituo cha polisi cha Sinza saa mbili asubuhi na nimuulizie Inspekta Amour.
 
ITAENDELEA

No comments:

Post a Comment