Saturday, November 19, 2016

WAJASIRIAMALI KAZI ZA MIKONO MKINGA MKOANI TANGA WAPEWA SOMO



Tangakumekuchablog
Mkinga, WAJASIRIAMALI wanawake Tanga wametakiwa kulitumia soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kutafuta masoko na kuacha kutegemea masoko ya ndani ambayo hayawezi kuwatangaza.
Akizungumza kwenye kongamano la Wajasiriamali Wanawake kijiji cha Gombero Tarafa ya Maramba juzi, Mratibu wa Taasisi ya Maendeleo ya Wanawake (Inuka), Devid Msuya, alisema wajasiriamali wengi hawana uelewa wa soko la pamoja.
Alisema wako wajasiriamali wa kazi za mikono ambao bidhaa zao ziko na masoko nje ya nchi lakini kutozitangaza kwao zimekuwa zikishilizia mikononi na kushindwa kutangazika.
“Soko la pamoja lipo muda mrefu toka lifunguliwe lakini la kushangaza ni kuwa wajasiriamali wa ndani hawana uelewa wa kulitumia na badala yake wenzao wamekuwa wakilitumilia ipasavyo” alisema Msuya na kuongeza
“Hebu tulichangamkie kwani soko hili ndio la kuzitangaza kazi zetu za mikono na tukiendeleza kulala wenzetu watahozi hadi masoko yetu ya ndani” alisema
Alisema kwenye soko hilo la pamoja kuna fursa nyingi za kujiendeleza ikiwemo kubadilishana uzoefu na mbinu za kibiashara na kuweza kufikia kuwa mjasiriamali wa Kimataifa.
Kwa upande wake mjasiriamali wa kutengeza mikeka na ungo, Mwanahawa Mbelwa, alisema kutokuwa na vikundi imekuwa chanzo cha kazi zao kutojulikana.
Alisema awali waliunda vikundi  na kufa kutokana na kushindwa kupata mikopo hivyo kuzitaka taasisi za fedha na mashirika   kutoa  elimu ya vikundi ili kupata mikopo isiyo na riba.
“Hapa tuko wajasiriamali tofauti ambao  kama tutapatiwa mikopo na elimu ya ujasiriamali na kuunda vikundi tunaweza kuwa wajasiriamli wakubwa na kuliteka soko la pamoja” alisema Mbelwa
Aliwataka wajasiriamali wenzake kuunda vikundi na kuweza kupata mikopo katika taasisi za fedha ili kuweza kuzifanya kazi kwa weledi na kuweza kuyafikia masoko ndani ya Jumuiya Afrika Mashariki.
                                                    Mwisho

No comments:

Post a Comment