Sunday, November 20, 2016

UFUNGUZI LIGI YA AZAM FEDERESHENI CUP YAANZA KWA VITUKO


Tangakumekuchablog
Tanga, UFUNGUZI wa ligi ya Azam Federeshen Cup iliyozinduliwa leo uwanja wa Mkwakwani Tanga umegubikwa na fujo za washabiki baada ya timu ya Muheza United kufunga goli la pili lililoipa ushindi wa pointi tatu.
Ugunguzi huo wa mashindano uliofunguliwa na Makamo wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, Walles Karia na viongozi mbalimbali wa mpira ngazi ya Taifa na Mkoa ulizikutanisha timu ya Muheza United na Safi Politan kutoka Dar es Salaa.
Timu ya Muheza iliibuka na ushindi wa mabao 2 kwa 1 na kuibua shangwe kwa washabiki wa timu hiyo na kulazimika polisi kuwadhibiti washabiki.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo , kocha wa Safi Polistan, Mussa Rashid, alisema vijana wake walicheza chini ya kiwango na kuruhusu mabao kurejeshwa kwa urahisi.
Alisema kipindi cha kwanza walicheza vizuri na kuonyesha dalili za kuongeza magoli mengine lakini goli moja wachezaji wake walibweteka na kukubali kurejeshwa kwa urahisi.
“Wachezaji wangu walibweteka baada ya kupata goli la kwanza lililoenda hadui kipindi cha pili, wenzetu kipindi cha pili walikuwa mbogo na kutuchanganya” alisema Rashid
Kwa upande wake, kocha wa Muheza United, Lukindo Domonic, alisema wenzao waliwabeza na kuona timu za Tanga ni za kunyakuwa pointi tatu na kuondoka zao.
Alisema wakati walipoenda katika vyumba vya kupumzika aliwaeleza wachezaji wake wanapaswa kugangamala kuondosha dhana ya kufanywa uwanja wa Mkwakwani kama shamba la bibi.
“Niliwaeleza wakati tuko katika vyumba vya kubadilisha nguo kuwa wanapaswa kukomaa ili kuondosha aibu mbele ya umati uliojitokeza uwanjani” alisema Lukindo
Alisema kwa ushindi huo wa ufunguzi umewatia morali na ari ya  ushindi  katika michezo iliyoko mbele yao na kuwapongeza vijana wake ambao awali wapinzani waliwabeza.
                                                    Mwisho


Makamo wa Rais Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania, Walles Karia, akisalimia na wachezaji wa timu ya Muheza United ya Tanga  na Sifa Politan kutoka Dar es Salaam wakati wa ufunguzi michuano ya Azam Federetion Cup iliyozinduliwa Mkwakwani leo.






Polisi wa kutuliza Ghasia (FFU) akimdhibiti shabiki aliedhaniwa kuwa ni wa timu ya Muheza United ambaye alikuwa akifanya fujo baada ya timu yake kufunga bao la pili na kutaka kuingia uwanjani  wakati wa mchezo ligi ya Azam Federeshen Cup uliofanyika leo uwanja wa Mkwakwani Tanga.

No comments:

Post a Comment