Tuesday, November 22, 2016

LEICESTER YAENDELEZA UBABE UEFA

UEFA: Leicester City wang'ara mbele ya Club Brugge

Leicester iliutawala vyema mchezo huo
Leicester city wamepata ushindi maridhawa wakati wa muendelezo wa ligi ya mabigwa barani Ulaya baada ya kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya club Brugge.
Leicester wanahitaji alama moja tu kutinga hatua ya mtoano.

Mchezaji Shinji Okazaki alimaliza vyema kazi ya Christian Fuchs na kuandika goli la kwanza kwa kikosi hicho kinachonolewa na Muitaliano Claudio Ranieri.
Riyad Mahrez akaongeza goli la pili kwa penati murua ikiwa ni goli lake la nne ndani ya ligi ya mabigwa baada ya Marc Albrighton kuangushwa ndani ya eneo la hatari.
Leicester city hawashikiki katika ligi ya mabingwa Ulaya huku wakiwa wanaboronga EPL.

Matokeo ya michezo mingine

Monaco 2-1 Tottenham
Borussia Dortmund 8-4 Legia Warsaw
Sporting 1- 2 Real Madrid
CSKA Moscow 1- 1 Bayer 04 Leverkusen
FC Copenhagen 0-0 FC Porto
Dinamo Zagreb 0-1 Olympique Lyonnais
Sevilla 1- 2 Juventus

No comments:

Post a Comment