Friday, November 25, 2016

WAKUU WA IDARA, WATUMISHI WAPEWA SOMO NA NAIBU WAZIRI SULEIMAN JOFFO



Tangakumekuchablog
Tanga, NAIBU Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Suleiman Joffo, amewataka wakuu wa Idara na Watendaji maofisini kufanya kazi na kuacha ufanyaji kazi wa mazoea.
Pia alikemea baadhi ya wakuu wa Idara  kuwapandisha vyeo wafanyakazi kwa misingi ya urafiki na kuwahamisha watumishi kwa chuki.
Akizungumza na wakuu wa idara na wafanyakazi wa sekta mbalimbali jijini hapa jana, Joffo alisema kuna baadhi ya wakuu wa Idara wamekuwa wakizifanya ofisi kama mali zao hivyo kuwataka kubadilika.
Alisema malalamiko hayo yamekuwa mengi na Serikali kulaumiwa  na kusema yoyote ambaye hatokuwa tayari kufanya uadilifu kuachia ngazi.
“Serikali inahuzunika kuona malalamiko ya wananchi yamekuwa yakiongezeka kuwalalamikia wakuu wa idara maofisini, kila siku nimekuwa nikisema huduma ni haki ya kila mwananchi” alisema Joffo na kuongeza
“Kama kuna mtumishi au mkuu wa idara anaona majukumu aliyopewa kwa kuomba mwenyewe yamemzidi ni bora aacie ngazi mapema kwani fagio likipita litakuw alinasafisha” alisema
Akizungumzia pesa za Serikali ilizotoa kwa halmashauri nchini kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyoo, Joffo alisema muda uliowekwa mwishoni mwa December ukipita bila kukamilisha wakurugenzi watawajibishwa.
Alisema amebaini baadhi ya halmashauri zimeshindwa kukamilisha agizo hilo la Serikali kwa kushindwa kimaslahi za pande tatu , Afisa elimu, Afisa manunuzi na Injinia.
“Kuna baadhi ya halmashauri hadi muda huu nikuweka maji mwaga mchanga hakuna lolote linaloendelea, tunatambua kuwa ni kugombea maslahi na hili niseme muda ukimalizika na hakuna kiliochofanyika ni uwajibishwaji” alisema Joffo
Aliwataka wakuu wa Idara na wafanyakazi wenye dhamana maofisini kuacha kufanyiana majungu na badala yake kufanya kazi kwa bidii na kuwahudumia wananchi kupata huduma bora.
                                             Mwisho



 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo, akikagua ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 1 . 6 inayojengwa na kampuni ya Hari Singh and Sons kwa ufadhili wa Bank ya Dunia. Barabara hiyo hadi kukamilika kwake itagharimu zaidi ya shilingi bilioni 2.




Injinia wa halmashauri ya jiji la Tanga, Arafati Kaniki, akimsomea taarifa ya ujenzi wa barabara ya Nguvumali hadi Kwaminchi, Naibu Waziri  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo, wakati wa ziara yake Tanga

No comments:

Post a Comment