MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AWAONGOZA WAOMBOLEZAJI KUUAGA MWILI WA MAREHEMU DKT. KIGODA KARIMJEE,LEO
Maafisa wa Bunge wakibebea Jeneza 
lenye mwili wa marehemu Dkt. Abdallah Kigoda, wakati ulipowasili kwenye 
viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam Oktoba 15, 2015 kwa ajili ya 
kuagwa. 
Spika wa Bunge Mama Anne Makinda, akizungumza kutoa salamu kwa niaba ya Bunge.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akishiriki na baadhi 
ya Waumini wa dini ya Kiislamu, kumswalia Marehemu Dkt. Abdallah Kigoda,
 aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, wakati wa swala hiyo 
iliyoswaliwa kwenye Msikiti wa Maamur uliopo Upanga jijini Dar es 
Salaam, leo asubuhi. Marehemu Kigoda anatarajia kuzikwa leo Jimboni 
kwake Handeni, mkoani Tanga.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za 
mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Waziri wa Viwanda na 
Biashara, Marehemu Dkt. Abdallah Kigoda, wakati wa shughuli ya kuagwa 
mwili huo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, 
leo Okt. 15, 2015. Marehemu Kigoda anatarajia kuzikwa leo Jimboni kwake 
Handeni, mkoani Tanga.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akitoa 
heshima za mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Waziri wa 
Viwanda na Biashara, Marehemu Dkt. Abdallah Kigoda, wakati wa shughuli 
ya kuagwa mwili huo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es
 Salaam, leo Okt. 15, 2015. Marehemu Kigoda anatarajia kuzikwa leo 
Jimboni kwake Handeni, mkoani Tanga.
Baadhi ya Wanafamilia wa marehemu Dkt. Kigoda.
Sehemu ya waombolezaji na Wabunge waliohudhuria shughuli hiyo ya msiba Karimjee.
   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo 
Pinda, wakijumuika na baadhi ya biongozi wa Kitaifa na Waombolezaji, 
kushiriki katika shughuli ya kuagwa mwili wa aliyekuwa Waziri wa Viwanda
 na Biashara, Marehemu Dkt. Abdallah Kigoda, iliyofanyika leo Okt. 15, 
2015 kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mufti 
Mkuu wa Tanzania Abubakary Zubeiry, wakati alipowasili kwenye Msikiti wa
 Maamur uliopo Upanga jijini Dar es Salaam, leo asubuhi kwa ajili ya 
kuswalia mwili wa marehemu Dkt. Abdallah Kigoda, aliyekuwa Waziri wa 
Viwanda na Biashara, aliyefariki dunia majuzi Hospitali ya Apollo nchini
 India, alipokuwa amelazwa akitibiwa. Marehemu Kigoda anatarajia kuzikwa
 leo Jimboni kwake Handeni, mkoani Tanga.










 
No comments:
Post a Comment